• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali Yawataka wananchi kutoa ushirikiano katika elimu

Posted on: May 1st, 2019


Serikali yawataka wananchi kutojitenga na jukumu la kuondoa changamoto Shuleni Serikali imesema  inatambua  ukweli  wa namna taasisi zake hususani sekta ya elimu ilivyo na changamoto zinazokwamisha  upatikanaji wa haraka wa maendeleo lakini haiwezi kuziondoa kwa wakati mmoja.

Hivyo imewataka wananchi  kutambua  ushiriki wao wa kuchangia fedha za miradi mbalimbali shuleni utawezesha Serikali  kufanikisha kuziondoa changamoto  hizo  kwa urahisi na watoto wao kupata elimu bora kwa shule za umma.

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Elimu  Taaluma Mkoa wa Mwanza, Joseph Ngoseki, aliyemwakilisha Afisa Elimu mkoa huo, Michael Ligola katika mdahalo wa wazi kujadili  huduma ya elimu  inavyotolewa katika shule za msingi   na  sekondari za umma.

Mdahalo huo ulioandaliwa na Taasisi ya  Ilemela District CSOS Network (ILEDICNET)  ulihudhuria na vongozi mbalimbali wa Serikali, wadau wa elimu na wananchi ambapo walisema bado shule za serikali zinakabiliwa na changamoto kadhaa zikiwamo ni  uhaba wa vyumba vya  madarasa ya awali na msingi.

Pia upungufu wa matundu vya vyoo,  vitabu vya kiada, madawati, kukosekana kwa huduma ya maji shuleni, chakula, usiri juu ya mapato na matumizi ya shule, mahusiano mabaya kati ya jamii na walimu, shule kutokuwa na vifaa vya kujikinga na majanga  ya moto, upungufu wa walimu sambamba na walimu kutopandshwa madaraja na mengine mengi.

Akijibu hoja za wachangiaji, Ngoseki alisema ni kweli shule za  Serikali zina mapungufu yaliyotajwa lakini si rahisi  kuondoa changamoto hizo kwa wakati mmoja ispokuwa zitakwisha  endapo wananchi  watajitolea kwa nafasi yao kwa kuchangia fedha.

“Wananchi wanapaswa kuelewa hizi shule ni zao na ndio maana zinasimamiwa na kamati au bodi za shule ambaqpo wajumbe wake wanatokana na wananchi hao hao, sasa ili tuziondoe changamoto hizo ni lazima tushirikiane kwa pamoja, mfano hivi sasa kuna upungufu wa  vyumba vya madarasa kinachotakiwa ni wananchi wajenge boma na serikali itaezeka.

“Sasa jamii ikisubiri Serikali ifanye kila kitu tutachelewesha maendeleo ya sekta ya elimu, binafsi naipongeza Halmashauri ya Ilemela ambayo viongozi wake na wananchi wamejipangia utaratibu wao kwamba  katika kumaliza kero ya madarasa, wananchi wanajenga msingi, mbunge anayesimamia boma na halmashauri inaezeka, leo hii Mkoa wa Mwanza tunawatolea mfano kwa kuwa na miradi mengi.

“Najua kuna mapokeo hasi kwa wananchi juu ya kauli ya elimu bure kitendo ambacho kinasababisha kutochangia, usahihi ni kwamba Serikali imesema elimu ni bure bali ni elimu msingi bila malipo, hivyo wananchi wanapaswa kutambua michango ya maendeleo  katika shule zao ipo, ni muhimu kujenga nyumba za walimu, vyoo  pia wana jukumu la kusimamia  na kuhoji fedha zinazoletwa na Serikali kupitia kamati za shule,”alisema.

Naye Meya wa Halmashauri ya Ilemela, Renatus Muruga, alisema hadi sasa halmashauri hiyo imeweza kujenga misingi 92 ya vyumba vya madarasa, maboma  90 yamekamilika na kati ya hayo 31  yameezekwa  ambapo Mbunge wa Jimbo la Ilemela, Mhe.  Angelina Mabula (CCM) ametoa matofali 485,000 kwa  vyumba vya madarasa, nyumba za walimu na vyoo.

Muruga aliwataka wananchi kuelewa maana ya Serikali ni  wewe na mimi  ikiwa na maana watu wote hivyo kila mmoja anapaswa kuwajibika kwa nafasi yake.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Buhongwa, Sarah Ngwani (CCM)  alipongeza taasisi ya Iledicnet kwa kufanya utafiti na kuandaa mdahalo huo ambao umesaidioa Serikali kutambua changamoto zinazokabili shule zake na kuwataka wananchi kuungana na viongozi kusaidiana kuzitatua.

 Naye Mratibu wa Iledicnet , Nicas Nibengo, alisema ikiwa serikali itaweza kutatua mapunfufu yaliyopo katika shule zake, hakika zitaleta ushindani mkubwa dhidi ya  shule binafsi.

“Vile vile tunashauri jamii ielimishwe juu ya kuchangia kwani imebainika imepokea kauli ya Serikali elimu bure kwa mtazamo tofauti, wito kwa Serikali kuweka mikakati ya kuhakikisha vyumba vya madarasa vinapatikana ili kuepusha wanafunzi kulundikana katika darasa moja, vile vile kuongeza walimu wa kutosha katika shule zake, vinginevyo ubora wa elimu utaendelea kushuka.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.