• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali Yazindua vivuko vya Bugorola- Ukara,Chato- Nkome

Posted on: August 25th, 2019


Serikali  imezindua rasmi ujenzi wa vivuko viwili  vya kisasa  vitakavyofanya safari za kusafirisha abiria , mizigo na magari  kati ya Bugorola-Ukara   Wilaya ya Ukerewe  Mkoa wa Mwanza na Chato-Nkome Wilaya ya Chato mkoani Geita.


Uzinduzi huo umefanyika mkoani Mwanza eneo la karakana ya Kampuni ya Songoro Marine Transport Boaty  Ltd, inayojenga vivuko hivyo ambapo viongozi mbalimbali wa Serikali kutoka Chato  na Ukerewe  walihudhuria hafla hiyo.


Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme (Temesa), Mhandisi Japhet Masele alisema Serikali imeamua kujenga vivuko hivyo kutokana na kuwapo na mahitaji makubwa hususani Ukerewe ambapo hivi karibuni kulitokea ajali  eneo la Bugorola na kusababisha vifo  vya watu.


Mhandisi Masele alisema  kivuko cha Bugorola-Ukara   kitajengwa  na Kampuni  ya Songoro Marine Transport Boaty  Ltd kwa Sh. bilioni 4.2 bila kuwapo na Ongezeko la Thamani (VAT) huko kile cha  Chato- Nkome kitagharimu Sh bilioni 3.1.


“Vivuko vyote vitagharimu Sh bilioni 7.3 ambazo zote zitatolewa na Serikali, kwa mujibu wa mikataba tuliyoingia na kampuni hii ni kwamba vivuko hivi vitajengwa kwa miezi 10 tu, hivyo tunamuomba mzabuni wetu  ambaye ni mzawa akamilishe kazi hii kwa wakati.

“Kivuko cha Bugorola-Ukara kitakuwa na na vipimo vya urefu wa mita 39, upana mita 10 na kitaelea ndani ya maji kati ya mita 0-7 hadi 1.0, pia kitakuwa na uwezo wa kubeba tani 100 yaani abairia 300, magari 10 na mizigo, vile vile kivuko cha Chato-Nkome kitakuwa na uwezo wa kubeba abiria 200, magari 10 na mizigo.


“Vivuko hivi  vitafungwa injini  mbili  na vitaendeshwa na mifumo  miwili ya usukani ambapo moja itakuwa ni ya dharula, kama mtakumbuka nimewaambia tunataka kuimarisha usalama majini na usafiri wa uhakika ndiyo maana vinajengwa kwa mabati maalum ya daraja la kwanza ‘grade  A marine’ hivyo natarajia  Aprili, 2020 tutakabidhiwa,’alisema.


Naye Mkurugenzi  Mtendaji wa Kampuni ya Songoro Marine Transport Boaty  Ltd,Major Songoro aliipongeza Serikali kwa kumwamini na kumpa zabuni za kujenga vivuko hivyo huku akiahidi kuvikabidhi Februari na si kama mkataba unavyoelekeza Aprili, 2020.


“Kutokana na Serikali kuwa na imani na mimi, naahidi kwamba vivuko hivi navikabidhi Februari, 2020 na si kama mkataba unavyosema nikabidhi Aprili, kama mnavyoona wafanyakazi wameanza kazi rasmi na wana utayari wa kufanya kazi, binafsi naogopa kusema mambo mengi bali nataka vitendo ndio viongee zaidi,”alisema.


Kwa upande wa Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Warioba Sanya amesema  ujenzi wa vivuko hivyo ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Mhe.Dkt. John Magufuli ya kutaka  kuboresha   na kuimarisha usalama wa abiria na vyombo vya majini ndani ya Ziwa Viktoria.


“Hapa kinachotekelezwa ni ahadi ya Rais wetu na ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), hatutaki yale yalitokea Bugorola yatokee tena, sote tunajua mahitaji yaliyopo pale Bugorola ingawa kuna kivuko  cha MV. Sabasaba kinafanya kazi pale.


“Kama Serikali  tumekusudia kuwawezesha wakandarasi wa ndani ili fedha hizo ziweze kubaki hapa hapa, pia Mwanza ipo katika mkakati maalumu wa kuwa kituo cha uchumi katika   Nchi za  Afrika Mashariki ndiyo maana tunataka kampuni hii iwezeshwe na kuwa mahiri kwa ajili ya kujenga meli kubwa hapa hapa Mwanza, hivyo tunawaomba viongozi wa kampuni hii wajitahidi sana katika kazi,”alisema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.