• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Shamba la Taifa la Mifugo Mabuki liwekewe miundombinu ya visima ili kuwa na Malisho bora: RAS Mwanza

Posted on: January 4th, 2024

Shamba la Taifa la Mifugo Mabuki liwekewe miundombinu ya visima ili kuwa na Malisho bora: RAS Mwanza


Leo Januari 4, 2024 Katibu Tawal Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana amefanya mazungumzo mafupi Ofisini kwake na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Daniel Mushi ambapo ametoa rai kwa Wizara hiyo  kuweka miundombinu ya visima vya Maji kwenye Shamba la Mabuki ili uoteshaji wa Malisho uwe endelevu.

Balandya amesema mradi huo uliopo Wilayani Misungwi ambao umewalenga vijana kujikwamua kiuchumi kwa kuwa wafugaji bora ni mzuri ila changamoto iliyopo ya uhaba wa maji unarudisha nyuma malengo yaliyokusudiwa na Wizara.

"Ndugu Naibu Katibu Mkuu, wakati wa kiangazi suala la Malisho linakuwa tatizo kutokana na uhaba wa malisho na kufanya mifugo kushuka ubora wake na kushindwa kupata soko",amefafanua Mtendaji huyo wa Mkoa wakati wa mazungumzo mafupi na Mtendaji huyo wa Wizara sekta ya mifugo.

Balandya amebainisha kuwa Ofisi yake hivi sasa ipo mbioni kukamilisha Maduka maalum ya nyama yapatayo matano ili kuwahakikishia soko vijana hao wa Mabuki walipo kwenye Mradi wa Jenga kesho iliyo bora (BBT).

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu Prof. Mushi amesema changamoto zilizopo katika shanba hilo Wizara inazitambua likiwamo tatizo sugu la uvamizi kutoka kwa wananchi na sasa wapo mbioni kuweka ulinzi wa kudumu kutoka Suma JKT.

"Nakuhakikishia Ras tutaanza kuwaondoa wavamizi wote hivi karibuni na kuweka ulinzi wa kudumu,tutaboresha nyumba za kulala za vijana wanaendelea kuingia kwa awamu kupata mafunzo kwenye vituo atamizi,na pia suala la visima litapatiwa ufumbuzi muda siyo mrefu," Naibu Katibu mkuu.

Ameongeza kuwa mradi huo ni jicho la Mhe Rais Samia ambaye ndoto yake ni kuona kundi la vijana wanaokosa ajira wanakombolewa na mradi huo ambao umewekewa mikakati yenye tija.

"Upo mfuko maalum ulio na Shs bilioni 130 ambao utaingizwa kwenye baadhi ya Taasisi za kibenki ili kuwakopeaha vijana hao mara baada ya kupata mafunzo hayo ya unenepeshaji mifugo lengo likiwa wawe wafugaji bora na siyo wachungaji",amesisitiza Naibu Katibu mkuu huyo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.