• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SHULE MPYA YA GHOROFA KATA YA MHANDU KUMALIZA MSONGAMANO WANAFUNZI DARASANI

Posted on: January 29th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 29 Januari, 2026 amekagua na kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa shule mpya ya Sekondari kwa mfumo wa ghorofa mtaa wa Kasota, kata ya Mhandu Wilayani Nyamagana.

Akizungumza na wananchi kwenye hafla hiyo Mhe. Mtanda ameipongeza serikali kwa kutoa fedha na Uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza kwa maendeleo ya kasi katika sekta ya elimu na kwamba kuanzia mwaka 2021 hadi sasa kumekua na ongezeko la shule za sekondari 58 kutokana na juhudi zao.

Aidha, ameiagiza Halmashauri hiyo kutoa fedha Tshs. Milioni 200 na kusimamia kwa kasi ukamilishaji wa ujenzi wa shule hiyo hadi kufikia mwezi desemba mwaka huu ili mapema mwezi januari mwakani wanafunzi waanze kusoma katika madarasa ya shule hiyo mpya na kusaidia kuondoa msongamano kwenye shule mama.

Halikadhalika, amewataka MWAUWASA na TANESCO kuhakikisha wanafanikisha huduma za Maji na Umeme kwenye shule hiyo mpya ili kuongeza kasi ya ujenzi na pia kwenda sambamba na ujenzi wa miundombinu mara ujenzi utakapokamilika wanafunzi waanze kuyatumia bila kusubiri huduma za msingi.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema shule hiyo itakapokamilika itachukua wanafunzi 1620 na itasaidia Kata hiyo kuwa na shule mbili za sekondari na kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani pamoja na kupunguza umbali kwa wanafunzi kwenda Mhandu sekondari.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mhandu Warioba Marato amesema Mwezi Juni 2025 Serikali ilitoa Tshs. Milioni 584.2 kwa ajili ya kujenga Shule ya sekondari ya kawaida katika kata hiyo lakini kutokana na ongezeko la wanafunzi kuwa kubwa halmashauri iliamua kujenga kwa mfumo wa ghorofa.

Mwalimu Marato ameongeza kuwa mnamo Mei 2025 kibali kilitolewa na kuanza rasmi kwa ujenzi wa shule hiyo kwa mfumo wa ghorofa katika mtaa wa Kasota na hadi kukamilika wanahitaji nyongeza ya Tshs. Bilioni 1.56 ambapo sasa ujenzi umefikia 45%.

Halmashauri ya wilaya ya Nyamagana kwa mwaka 2026 wanafunzi 13609 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha kwanza na mpaka sasa wanafunzi 10195 wameripoti shuleni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • NYANZA YATAKIWA KUHAKIKISHA PEMBEJEO ZA PAMBA ZINAWAFIKIA WAKULIMA KWA WAKATI

    January 30, 2026
  • WAKULIMA WATAKIWA KUTUMIA MFUMO WA STAKABADHI ZA GHALA KUKUZA UCHUMI

    January 30, 2026
  • USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO UNAHITAJI UWAJIBIKAJI WA PAMOJA

    January 30, 2026
  • WANANCHI MWANZA WATAKIWA KUCHANGAMKIA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 30, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.