• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Somo la Michezo lifundishwe Shuleni ,Vyuoni – Majaliwa

Posted on: June 9th, 2018

Somo la  Michezo lifundishwe Shuleni ,Vyuoni – Majaliwa

Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa amesema kuwa somo la elimu ya Michezo linatakiwa kufundishwa kuanzia shule za msingi,sekondari hadi vyuo vikuu ili kukuza viwango vya michezo na vipaji kwa vijana Tanzania.


Mhe. Majaliwa alisema hayo  Mkoani Mwanza katika uwanja wa CCM Kirumba, wakati akifungua rasmi mashindano ya shule za Sekondari na  msingi( UMISSETA na UMITASHUMTA) Taifa kutoka Mikoa 26 ya Tanzania bara na Mikoa 2 kutoka Unguja na Pemba Zanzibar.


“Kauli mbiu yetu mwaka huu katika  Mashindano ya umiseta na umishumitani,Michezo, Sanaa na Taaluma ni Msingi wa maendeleo ya wanafunzi katika Taifa letu,”alisema Majaliwa.


Mhe. Majaliwa aliongeza  kuwa Serikali imeweka kipaumbele katika suala la  michezo mashuleni,huku akizitaka Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia,  kushirikiana na Wizara ya Habari,Utamaduni Sanaa na Michezo kuhakikisha somo la michezo linafundishwa kuanzia shule za msingi, Sekondari hadi vyuo vikuu ikiwa lengo ni kukuza kiwango cha michezo Nchini na vipaji kwa vijana.


Aliziagiza Halmashauri zote Nchini kuhakikisha zinatenga bajeti kwa  ajili ya michezo katika shule za msingi na Sekondari na kuwapa fursa walimu wenye uwezo wa kufundisha michezo shuleni ,badala ya kuwapa bora walimu kufundisha somo hilo.


Waziri Majaliwa amewaonya maofisa Elimu na walimu wa michezo mikoani kutohujumu mashindano hayo kwa kuingiza watu wasio wanafunzi kushiriki ambao ni ’’ Mamluki”kuwa wakigundulika wamefanya hivyo hatua kali dhidi  yao zitachukuliwa na Serikali.

Awali naibu Waziri Ofisi ya Rais Tamisemi Dkt. Leonard Akwilapo amesema kuwa mashindano hayo yamelenga kuibua wanamichezo nchini kutengeneza ajira ambapo tayari baadhi ya vijana wamefanikiwa kutokana na michezo.


Mhe. Akwilapo amesema mfano wa  wachezaji wa mpira wa miguu ambao wamefikia kiwango bora waliotokana na michezo shuleni ambao ni Edibily Lunyamila aliyewahi kuchezea timu ya Yanga, Shiza Kichuya ambaye ni mchezaji nyota wa Simba na Mbwana Samatta ambaye kwa sasa yuko nchini Ubeligiji akichezea timu Genk iliyopo ya ligi kuu .

Naye Mwalikishi wa kampuni ya COCA COLA ambao ni wadhamini wa mashindano hayo ,David Kalamagi wameahidi kuendelea kudhamini mashindano hayo na kufanya maboresho kwenye baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza wakati wa  mashindano hayo.


Mashindano hayo ya Umiseta na Umitashumita yameshirikisha jumla ya wanafunzi 6480 kutoka mikoa yote ya Tanzania bara na visiwani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.