• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Tuendelee kuchukua tahadhari dhidi ya mlipuko wa Kipindupindu: Dkt.Rutachinzibwa

Posted on: January 20th, 2024
  • Tuendelee kuchukua tahadhari dhidi ya mlipuko wa Kipindupindu: Dkt.Rutachinzibwa


Leo Januari 20, 2024 Mganga mkuu wa mkoa wa Mwanza Dkt.Thomas Rutachunzibwa amekutana na makundi maalum kwa lengo la kuwapatia elimu na kuwataka kuchukua tahadhari zote dhidi ya mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu ikiwemo ulaji wa chakula cha mkusanyiko wa watu wengi.

Akizungumza nao kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa, amesema baadhi ya wagonjwa waliofuatiliwa walibainika kupata maambukizi hayo kutoka msibani hivyo ni vyema kuwa makini eneo hilo kwa kunawa maji yanayo tiririka na kuepuka kwa kipindi hiki kulala matanga.

"Ni lazima kila mmoja wetu atambue kilicho mbele yetu kwa sasa na tuzingatie usafi kwenye maeneo yanayo tuzunguka tukuzingatie yote haya visa vya mlipuko vitatoweka", amesisitiza Mganga Mkuu wa Mkoa.

Amesema tusiache jukumu hili kwa Serikali pekee bali kila mmoja awe makini na kutoa elimu hii kwa wengine ili jamii iendelee kubaki salama na kuendelea na majukumu ya  ujenzi wa Taifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana aliyehitimisha mafunzo hayo mafupi ya utoaji elimu kwa makundi maalum amesema Kipindupindu kinapona endapo mgonjwa aliyebainika atafikishwa mapema kwenye vituo vya afya vilivyotengwa na matibabu yake ni Bure hivyo jamii yote izingatie miongozo yote ya tahadhari inayotolewa na wataalamu wa afya kwa lengo la kulinda nguvu kazi ya Taifa isipotee.

By

"Huu ni ugonjwa wa aibu yaani mtu kula kinyesi kibichi kinachotokea na vimelea,naamini mafunzo haya ya leo mliopatiwa yatakuja na matokeo chanya",Mkuu wa Wilaya Nyamagana.

Mratibu wa elimu ya afya kwa umna Mkoa wa Mwanza Leonald Mlyakado amebainisha Serikali inaendelea na zoezi la uelimishaji na kukagua maeneo yote yenye viashiria hatarishi na ugonjwa huo na kuchukua hatua za kitaalamu.

Mmoja wa wanufaika na elimu hiyo Alfred Kapore ameishukuru Serikali kwa utoaji wa mafunzo hayo kwani baadhi walikuwa hawana ufahamu wa kutosha kumtambua mgonjwa wa Kipindupindu na tahadhari nyingine.

Makundi hayo maalum yaliyonufaika na elimu hiyo ni walemavu,vijana,wanawake,wafanyabiashara wadogo na maafisa usafirishaji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.