Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Usalama wa Wananchi ni Kipaumbele changu- RC MAKALLA

Posted on: May 31st, 2023

*Usalama wa Wananchi ni Kipaumbele changu- RC MAKALLA*


*Aomba Ushirikiano kufanikisha Maendeleo mkoa wa Mwanza*


*Atangaza ratiba ya Usikilizaji Kero za wananchi Jimbo kwa Jimbo*


*Awataka watumishi kujibu kero za wananchi kwa wakati*


*Aagiza uimarishwaji wa Mapato ya ndani na Idara ya Ardhi isimame imara kutatua kero*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Amos Makalla amewataka viongozi wa wilaya ya Ilemela kusimamia masuala ya Usalama wa jamii ili wananchi wawe huru kufanya kazi za kujitafutia maendeleo.

CPA Makalla amebainisha hayo mchana wa leo Mei 31, 2023 kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela alipofika kujitambulisha kufuatia kuhamishiwa kwake na Mhe. Rais Mkoani Mwanza mapema mwezi huu.

"Watu wakikosa usalama watakosa amani ya kufanya mambo ya Maendeleo hivyo lazima tukumbushane umuhimu wa kuwa na amani kwenye maeneo yetu ili kuleta tumaini kwa wananchi kuwa wapo huru kujitafutia kipato." Amesema Makalla.

Aidha, Mhe. Makalla amesisitiza nidhamu ya kazi kwa watumishi ili wananchi wapate huduma bora na kuiamini serikali yao na kuondoa hofu na dukuduku kwa watumishi wa umma.

"Mkiwahudumia vyema mwananchi wataipenda Serikali na kinyume chake wataichukia hivyo tuepushe migogoro na migongano kwenye maeneo yenu ya kutolea huduma." CPA Makalla.

Vilevile, ameiagiza Halmashauri hiyo kusimamia kwa dhati ukusanyaji wa mapato ya ndani ili wawe na rasilimali za kutosha kutekeleza miradi mbalimbali kwa jamii na kwamba wote kwa pamoja ni lazima wadhibiti Mapato ya ndani na wajiwekee utaratibu wa kujibu Hoja za Ukaguzi kwa wakati.

"Hakikisheni fedha zote zinazokusanywa zinakwenda Benki ili tuweze kujihakikishia ukusanyaji mzuri na  kuwahudumia wananchi kwa kutekeleza miradi mbalimbali na wabadhirifu wa fedha wajue kabisa kuwa tunawafuatilia" Amesisitiza.

Aidha, amewaagiza viongozi na watumishi kujibu kero za wananchi kwa wakati na kutosubiri ofisini bali wawafuate kwenye makazi yao na kwamba atafanya ziara ya kusikiliza kero za wananchi kwenye kila wilaya na atawapima wetakaobainika kuwa na kero nyingi.

"Nimekuja kuwasalimia na kujitambulisha kwenu hivyo naombeni sana ushirikiano wenu Viongozi, waheshimiwa Madiwani na watendaji wote tufanye kazi kwa pamoja ili kwenye mafanikio tuwe pamoja na kwenye Changamoto tuwe pamoja pia, hodi Mwanza." Mhe. Makalla.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela Mhe. Hassan Masala amesema wilaya hiyo unaendelea kuboresha mazingira kwa kuwaletea huduma bora za Miundombinu, Elimu na Afya na kwamba makundi yote yanawezeshwa vema kupitia idara ya Maendeleo ya Jamii.

Aidha, amebainisha kuwa kwa Mwaka wa fedha inayoendelelea (2022/23) Halmashauri ya Wilaya ya Ilemela imekadiria kukusanya Shilingi Bilioni 13 na hadi sasa wamekusanya zaidi ya bilioni 14 ambayo ni sawa na asilimia 109 na wanaendelea kutekeleza Miradi yenye thamani ya Bilioni 18.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.