• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

VIJANA ZIDISHENI UBUNIFU ILI MKUZE KIPATO UFUGAJI WA SAMAKI KISASA: RC MTANDA

Posted on: December 10th, 2024

VIJANA ZIDISHENI UBUNIFU ILI MKUZE KIPATO UFUGAJI WA SAMAKI KISASA: RC MTANDA


Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Mh. Christopher Ngubiagai amewataka vijana wanaojishughulisha na ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba kuzidisha ubunifu katika mradi huo ili kukuza mtaji na kuongeza kipato chao.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na vijana hao mapema leo  asubuhi Disemba 10,202  eneo la Kisoko kata ya Luchelele wakati wa zoezi la uvunaji wa samaki tani 2 kikundi cha Isingiti, Mh. Ngubiagai amebainisha uchumi wa bluu hivi sasa umekuwa mkombozi kwa vijana hivyo kazi iliyopo sasa ni kupanua wigo utakaosaidia kusonga mbele kimaendeleo.

"Serikali ya Rais Dkt.Samia imeweka mazingira mazuri katika sekta hii ya uvuvi,mikopo inayotolewa na benki ya TADB ni nafuu,hakuna tena sababu ya vijana kukaa vijiweni badala yake ni kuchangamkia fursa hii ili kujiletea maendeleo",Mkuu wa wilaya.

Aidha amevipongeza vikundi vya vijana hao kwa nidhamu ya urejeshaji wa mikopo kwa asilimia 100 hali inahofanya kuwepo kwa mzunguko mzuri kwa wakopaji wengine.

"Ndugu mgeni rasmi leo unashuhudia uvunaji huu wa samaki uliotokana na mkopo kutoka benki ya TADB wa zaidi ya shs milioni 122 uliotuwezesha kununua vizimba 8 kwa gharama ya zaidi ya shs milioni 33 na kupandikiza vifaranga 80,650 vilivyogharimu zaidi ya shs milioni 14,"Omari Mangu,Katibu wa kikundi.

Kwa upande wake Meneja wa benki ya TADB Kanda ya ziwa Samson Siyengo amesema jumla ya shs bilioni 4 zimetolewa kwa vikundi vya ufugaji wa samaki mkoani Mwanza na awamu ijayo watatoa shs bilioni 5.

Mradi wa ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba ulizinduliwa rasmi na Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan Januari 30,2024 kwenye uwanja wa Nyamagana mkoani Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.