• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

VYAMA VYA USHIRIKA VYATAKIWA KUTUMIA MIFUMO YA TEHAMA

Posted on: October 21st, 2024

VYAMA VYA USHIRIKA VYATAKIWA KUTUMIA MIFUMO YA TEHAMA


Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde (MB) amewataka viongozi wa vyama vya ushirika kutumia mifumo ya kisasa ya Tehama na kuacha kufanya kazi kwa kutumia mifumo ya zamani ili waweze kutoa huduma bora katika vyama.

Amesema hayo leo Oktoba 21, 2024 wakati akifungua maadhimisho ya siku ya kimataifa ya ushirika wa akiba na mikopo mwaka 2024 yanayofanyika Kitaifa Mkoani Mwanza katika viwanja vya Mirongo Wilaya ya Nyamagana.

Aidha Mhe. Silinde amesema ili kuweza kuleta maendeleo katika vyama vya ushirika viongozi wa vyama hivyo wanatakiwa kufanyakazi kwa kufuata sheria na miongozo.

" Viongozi waendelee kusimamia ushirika kwa kufuata misingi, kanuni, sheria na miongozo kwa ajili ya kuleta maendeleo"amesema Mhe. Silinde.

Kadhalika Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Mwanza Bwana Peter Kasele kwa niaba ya Katibu Tawala amewataka wananchi kutumia fursa ya maadhimisho ya siku ya kimataifa ya ushirika wa akiba na mikopo katika kujipatia elimu ya masuala ya fedha.

Sambamba na hayo bwana Kasele amesema kuwa Serikali ya Mkoa inatambua umuhimu na mchango wa vyama vya ushirika katika kuleta maendeleo kwa watumishi pamoja na wananchi.

Naye MwenyeKiti wa Bodi ya chama kikuu cha Ushirika wa Akiba na mikopo Tanzania SCCULT Mwl. Aziza Mshana amesema chama hicho kinashukuru kwa mchango wa Serikali katika kuthamini mchango wa ushirika wa akiba na mikopo katika kukuza uchumi.

Maadhimisho hayo yanafanyika kwa muda wa siku 5 kuanzia Oktoba 20, 2024 mpaka Oktoba 24, 2024 yenye kauli mbiu ya "Ulimwengu Mmoja kupitia Ushirika wa Kifedha" yanaadhimishwa kwa mara ya 76 Duniani na 15 kwa nchi ya Tanzania tangu kuanzishwa kwake.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.