WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI
Mganga Mkuu wa Mkoa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amewapa mafunzo mafupi waandishi wa Habari mkoani Mwanza juu ya njia za kutokomeza watoto wa mtaani mkoani humo huku akisisitiza maswala ya malezi kwa wazazi kuwa bora wakati wote hata kama kuna sintofahamu baina ya wazazii hao.
Ametoa mafunzo hayo Leo 29 Mei, 2025 katika ukumbi wa Ofisi ya Mganga mkuu wa mkoa Mwanza, huku akiwataka waandishi hao kutoa Elimu ya kutosha kupitia vyombo vyako vya Habari, pia kuhamasisha sheria za kutoa misaada zifwate katika jamii Ili kuweza kutokomeza Hali hiyo.
“Wapo wale ambao Wana uwezo hivyo misaada tunayotaka kutoa katika jamii tuwe tunafata Sheria na taratibuu Ili kuweza kufika pale tunataka, hivyo kwa pamoja naomba mtusaidie kutoa Elimu katika jamii na Sisi tunawaahidi ushirikiano” Amesema Jesca
Alikadharika, ameongeza kwa kuwataka wahusika wa kampeni hiyo kutokata tamaa na kuwa na moyo wa uthubutu ili kuja kuwa wa mfano katika nchi ya Tanzania, hivyo tushirikiane na serikali kuanzia serikali ya mtaa, kata na mpaka ngazi ya juu kwa kusambaza vipeperushi kwa wingi pamoja na kufanya vipindi kwa lengo la kusambaza ujumbe katika jamii.
Awali ya hapo, Afisa Ustawi wa Mkoa Ndugu Baraka Kona Kona akiweka bayana kuwa vyanzo vikuu vya kuongezeka kwa watoto hao ni migogoro ya kifamilia, Hali duni za kimaisha na ukosefu wa Elimu, amewataka waandishi wa Habari kuwa makini katika kuripoti Habari za watoto wa mtaani kwa lengo la kuongeza uelewaa katika jamii Ili kupunguza idadi wa watoto wa mtaani katika Mkoa wa Mwanza.
“Nawaomba waandishi wa Habari muwe mstari wa Mbele maana nyie ndio washika kamera hivyo mna nguvu kubwa ya kuweza kusambaza Elimu juu ya kutokomeza watoto wa mtaani “ Amesema Baraka.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive
S.L.P: 119, Mwanza.
Simu: 028-2501037
Simu ya Mkononi: 028-2501037
Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz
Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.