• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wakazi wa Sengerema wamuomba Jaffo awatembelee

Posted on: June 7th, 2019

Wakazi wa Kijiji cha Chifunfu  kilichopo wilayani Sengerema  Mkoa wa Mwanza wamemuomba Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Seleman Jaffo kufika katika wilaya hiyo ili kuona namna  watoto wanavyoteseka  kutembea umbali wa kilomita 19 kwenda  sekondari ya Chifunfu unaosababisha mimba nyingi kwa wasichana.

 Ombi hilo lilitoa juzi katika mkutano wa hadhara  uliofanyika eneo ilipojengwa Shule mpya ya Sekondari Bugumbisiko ambayo haijaezekwa vyumba sita vya madarasa.

Wakazi hao ambao ni, Janeth Japhet, Simeo Lubinza, Mathias Sweka walisema tangu diwani huyo achaguliwe amekuwa si kiongozi wa kutatua changamoto zao bali mambo yake binafsi kitendo ambacho kinasababisha watoto wao kupata mimba na kukatisha masomo hivyo kwa pamoja hawamtambui kama diwani wao.

“licha ya kujitolea kujenga shule nyingine ya sekondari ya Bugumbisiko imeshindwa kuezekwa na halmashauri ya Wilaya ya hiyo kwakuwa Diwani wa kata ya Chifunfu, Robert Madaha ndiyo anakwamisha jitihada zetu kutokana na itikadi za siasa”alisema Mathias Sweka

Vicent Magembe ambaye ni mjumbe wa serikali ya kijiji alisema diwani huyo hana nia nzuri na shule hiyo ambapo amekuwa akiweka vikwazo  ngazi ya wilaya ili shule hiyo isiezekwe, pia alidai kuwa taarifa za sekondari ya Bugumbisiko amekuwa akizificha na kutojadiliwa kwenye baraza.

Alisema  ndani ya kijiji hicho, watendaji wamekuwa wakibadilishwa mara kwa mara pale wanapoonekana kutomuunga ajenda zake, hivyo aliwataka wananchi kuwa na msimamo dhidi ya wakwamishaji maendeleo yao.

Akisoma taarifa za kamati ya ujenzi wa sekonadari ya Bugumbisiko, Katibu wa kamati hiyo,  Fredick Nyamwanda alisema wananchi waliamua kuanzisha ujenzi wa shule hiyo baada ya shule ya kata iliyopo sasa kujengwa mbali na kijiji hicho ambapo watoto hutembea kilimita 19 ili kuifika ambapo wengi hushindwa kumaliza masomo kutokana na mimba zinazotokana na vishawishi wanavyopata njiani.

Alisema   kutokana na adha hiyo, wananchi wa vitongoji vitatu kati ya tisa,  vya  Kijiweni, Mulumo na Luchanga waliamua kuanzisha ujenzi huo ambao vyumba sita vya madarasa vimekamilika huku nyumba ya mwalimu, maabara, jengo la utawala na ujenzi shimo la choo  ukiwa katika hatua za mwisho kukamilika.


“Mpaka sasa  ujenzi ulipofikia tumetumia sh. milioni 29.7  lakini kutokana na uongozi wa kijiji na kata kutokuwa karibu, kamati imepata wakati mgumu kupata pesa za kumalizia kutokana na kauli zinazotolewa na viongozi wetu, kwanza ujenzi huu umeingiliwa na siasa jambao ambalo limekatisha tamaa wananchi na wadau kutochangia,”alisema


Hata hivyo watendaji wa kata na vijiji walimtetea diwani huyo lakini zomea zomea ilizidi ambapo waliamua kukaa kimya na kumuomba diwani azungumze na wananchi wake.


Baadhi ya mabango yaliyokuwa yakionyweshwa mbele ya diwani  huyo yalisomeka ,  Mheshimiwa Rais Magufuli umbali wa shule ndio chanzo cha mimba Chifunfu, ‘Waziri Seleman Jaffo tuunge mkono kwani diwani wetu hajachangia hata 100 na shule hataki, tunakuomba ututembelee kwetu Chifunfu’.Bango lingine lilisomeka  kwamba ‘Rais  wetu tunakuunga mkono kwa asilimia 100, tuangalie elimu ndio msingi wa maendeleo, hapa kazi tu’.


Kwa upande wa diwani, Madaha alisema si kweli anakwamisha ujenzi huo kwani amekuwa akijitahidi kumshawishi Mkurugenzi wa Sengerema ili kuwaezekea madarasa hayo na hatimaye shule iweze kusajiliwa na kuanza masomo mwakani.


“Jamani binafsi nasikitika sana juu ya malalamiko yenu na uamuzi wenu wa kuniita mchawi wa maendeleo yenu, najua tatizo ni siasa  mnazichanganya na shughuli za maendeleo, kwanza mngejua ninavyopambana  juu ya shule hii msingekuwa mnanisema vibaya hivi, naombeni muache masuala ya mitaani ili tujenge shule hii”alisema Madaha


Aliongeza, “Kwanza niwahakikishie hadi sasa bajeti ya kuezeka madarasa haya imetengwa katika bajeti inayoanza Julai Mosi mwaka huu, hivyo niwaomba wote tuwe wavumilivu”


 MWISHO

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.