• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

‘Wamachinga’ Wakabidhiwa Vitambulisho 32 siku ya uzinduzi

Posted on: May 7th, 2018


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amewataka wafanyabiashara wadogo kutumia fursa ya kujisajili na kutambuliwa ili kuweza kulipa kodi itakayosaidia kujenga uchumi wa nchi ili nao waweze kukopesheka.

Mhe. Mongella ameyasema hayo wakati wa wazoezi la uzinduzi wa utoaji wa vitambulisho kwa wafanyabiashara wadogo wadogo (wamachinga) Mkoani humo, ili waweze kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa sheria na kuchangia pato la taifa.


“Kila mmoja wenu anayefanya biashara ndogondogo ana wajibu  kufanya hivyo isipokuwa kwa walio katika sekta rasmi ya biashara na kwa yoyote ambaye hata jisajili katika mfumo huo hataruhusiwa kufanya biashara kiholela”,alisema Mongella.


Naye Kamisha Mkuu Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Charles Kichere alisema tayari imevitambua vikundi 130 jijini mwanza ambavyo wanachama wake ambao ni wafanyabiashara wadogo wadogo wanatarajiwa kupatiwa vitambulisho.


Aidha, Kichere aliongeza kuwa jukumu kubwa ni kukusanya mapato na kutoa elimu ya ulipaji kodi, na zoezi hili la kutoa vitambulisho maalumu kwa machinga na kuendelea kulipa kodi kwa hiari, zoezi hili ni endelevu na mwaka huu wa fedha umeweka marekebisho madogo madogo ya kuwatambua machinga kwa kushirikiana na Nida, Rita na uhamiaji namba ya mlipa kodi na kitambulisho cha kitaifa.


Kwa upande wake  Naibu Kamishina kodi za ndani ufundi Michael Muhoja alisema tangu kuanza kwa zoezi hilo linafanyika nchi nzima na kwa Mkoa wa Mwanza wanatarajia kusajili vikundi 130,hadi sasa wameshatambua vikundi 37 vyenye jumla ya wafanyakazi 1,100 ambapo kwa uwakilishi wa siku hii ya uzinduzi wametoa vitambulisho 32.


Naye Said Tembo ambaye ni Mwenyekiti wa wamachinga Mkoani Mwanza amesema wanamshukuru Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kwa kuthamini juhudi zao na kuagiza wapatiwe vitambulisho ili waweze kutoa mchango wao kwenye ujenzi wa uchumi wa Taifa kwa kulipa kodi.


" Zoezi hilo liharakishwe ili wamachinga wote nchini waanze kulipa kodi kwa ajili ya maendeleo ya Taifa" alisema Tembo.


Awali Mstahiki Meya wa Jiji la Mwanza James Bwire akihututia wafanya biashara hao alisema Mkoa unakadiriwa kuwa na zaidi ya wafanyabiashara wadogo elfu 15 ambao wakitambuliwa na kupatiwa vitambulisho itaiwezesha mamlaka ya mapato Tanzania(TRA)kupanua wigo wa kodi.



Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.