• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANAHABARI, JESHI LA POLISI WAASWA KULINDA AMANI KIPINDI CHA UCHAGUZI

Posted on: August 7th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa rai kwa wanahabari nchini kuzingatia sheria, kanuni na miongozo ya kitaaluma ili kufikisha habari za ukweli na kuepuka kusababisha migogoro kwenye jamii hususani katika kipindi cha uchaguzi Mkuu wa 2025.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito huo leo tarehe 07 Agosti, 2025 alipokua akifunga semina ya siku moja kwa makamanda wa Jeshi la polisi pamoja na waandishi wa habari na watangazaji kutoka mikoa ya kanda ya ziwa kuelekea uchaguzi Mkuu wa 2025.


Amesema kwa pamoja wanahabari na jeshi la polisi wanapaswa kuelimisha jamii kuhusu sera za wagombea, kuibua na kufuatilia ukiukwaji wa sheria, kuhamasisha ushiriki wa makundi maalum kama walemavu na wanawake pamoja na kupambana na taarifa potofu na propaganda.


"Serikali imefanya jitihada katika kurekebisha sheria na sera ili kuhakikisha uhuru wa vyombo vya habari unalindwa ikiwa ni pamoja na marekebisho ya Sheria ya Huduma za Habari Sura ya 229 yaliyofanyika kwa ushirikiano na wadau ambayo imesaidia kuongeza uwazi, ufanisi na imani ya umma kwa tasnia ya habari." Mhe. Mtanda.


Aidha, amebainisha kuwa maboresho hayo yamepelekea kukua kwa tasnia hiyo hata kuwa na zaidi ya Magazeti 375, Vituo vya redio 247, Televisheni 68, Vyombo vya habari mtandaoni 355 na Blogu 72 nchini ambazo si tu kwamba zimesaidia kutoa ajira bali pia kupata jukwaa pana la upashanaji habari.


Vilevile, ameipongeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania pamoja na Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari kwa kuandaa mafunzo hayo muhimu katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi.


Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Habari Maelezo Rodney Thadeus amesema mafunzo hayo yamelenga kukumbushana kanuni na wajibu wa makundi hayo katika kulinda amani kwa kujenga taswira chanya kwa kamii ili wananchi waweze kutumia fursa ya utaifa wao kushiriki katika uchaguzi mkuu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • WANAHABARI, JESHI LA POLISI WAASWA KULINDA AMANI KIPINDI CHA UCHAGUZI

    August 07, 2025
  • RAS GEITA AWAALIKA WANANCHI KUJIFUNZA KILIMO CHA KISASA NANE NANE NYAMHONGOLO

    August 07, 2025
  • RAS GEITA AWAALIKA WANANCHI KUJIFUNZA KILIMO CHA KISASA NANE NANE NYAMHONGOLO

    August 07, 2025
  • WALIOBEBA MAFANIKIO YA MKOA KITAALUMA WAPONGEZWA

    August 06, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.