• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WANANCHI WA BUCHOSA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAJENGEA CHUO CHA UFUNDI STADI (VETA)

Posted on: November 10th, 2023

WANANCHI WA BUCHOSA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KUWAJENGEA CHUO CHA UFUNDI STADI (VETA)


*RC Makalla awaagiza TANESCO na RUWASA kupeleka huduma kuharakisha ujenzi huo*


*Halmashauri ya Buchosa kupata Chuo cha Kwanza*


*Mkuu wa Mkoa awataka vijana kujiandaa na fursa za ajira kutokana na ufundi watakaopata chuoni hapo*


Leo Novemba 10, 2023 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amevuka milima na mabonde kufika kwenye Kijiji cha Kayenze kilicho pembezoni mwa Mji wa Nyegunge kwenye halmashauri ya Buchosa kukagua ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi (VETA).


Akizungumza na wananchi kwenye eneo hilo la ujenzi Mhe. Mkuu wa Mkoa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zaidi ya Bilioni 3 kujenga chuo hicho ambapo amebainisha kuwa kitawajenga kiufundi katika fani mbalimbali vijana wa Buchosa na wilaya ya Sengerema kwa ujumla.

"Halmashauri ya Buchosa mmepata bahati sana, Rais Samia Suluhu Hassan anajenga vyuo kwenye halmashauri 63 kwa wakati mmoja ikiwemo na halmashauri yenu, nawapongeza sana kwa hili maana vijana wetu hapa watapata ujuzi kwenye fani mbalimbali ambapo itawasaidia kupata nafasi kwenye miradi ya ujenzi kama wa barabara" Makalla.

Makalla ametumia wasaa huo kuziagiza TANESCO na RUWASA kuhakikisha wanapeleka huduma za umeme na maji kwenye ujenzi huo ili kurahisisha shughuli zinazoendelea kwa kasi kwenye eneo hilo ambapo ndani ya wiki mbili tangia waanze ujenzi wamekwishafikisha asilimia 18 ya ujenzi.

"Umuhimu wa VETA hii ni mkubwa sana kwa vijana fani nyingi zitatolewa hapa kama umeme, mapishi, useremala, bomba na uashi hivyo itakua ni nafasi ya kijana kuamua asomee nini ili akajishughulishe mtaani kwenye kuinua uchumi wake." Amesisitiza Makalla.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya ya Sengerema Mhe. Dominic Makoye amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa kusimamia utekelezaji wa Ilani na ametoa wito kwa wataalam kuendelea kutoa ushirikiano kwenye kukamilisha mradi huo kwa manufaa ya vijana wa Buchosa.

Akizungumza kwa niaba ya wananchi, Diwani wa Kata ya Nyehunge Mhe. Dickens Kulwa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa mradi huo ambao ameutaja kuwa unawasaidia wananchi kupata fedha kutokana na shughuli ndogondogo wanazofanya kwenye mradi huo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.