• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Waziri Mkuu Majaliwa aipongeza Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza

Posted on: March 14th, 2023


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa ameipongeza Kamati ya Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza kwa kununua gari na kulikabidhi jeshi la polisi ili litumike kufanya doria mkoani humo.

Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa  ametoa pongezi hizo leo jijini Mwanza wakati akizindua Wiki ya Nenda  kwa Usalama Barabarani inayofanyika Kitaifa Katika Uwanja wa Furahisha Uliopo Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza baada ya Mwenyekiti wa Kamati hiyo Frednand Chacha kumkabidhi gari hilo aina ya Land Cruiser ili amkabidhi Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini(IGP) Camillus Wambura.

“Nitoe shukrani zangu za dhati kwa Kamati ya Mkoa ambayo imetoa gari na kulipa jeshi la polisi kwa ajili ya kufuatilia mwenendo mzuri wa matumizi wa vyombo vya moto hapa mkoani Mwanza hongera sana Mhe Mwenyekiti  wa Kamati Frednand Chacha kwa kushirikiana na kamati yako mmetumia fedha zenu na hatimaye gari limepatikana ambalo nimelipokea na kumkabidhi IGP.

“Natamani kila mwenye uwezo ambaye anaweza kuona umuhimu wa jeshi letu la polisi  katika kusimamia usalama wetu barabarani akafanya kama ilivyofanya Kamati ya Usalama Babarani Mkoa wa Mwanza, Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya usafiri na usafirishaji lengo letu ni kurahisisha shughuli za usafirishaji,”amesema Mhe.Majaliwa.


Aidha amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima kwa  kuunda kamati ambayo imeshirikiana na Kamati Kuu ya Kitaifa kuratibu maadhimisho hayo  kwani yatawanufaisha wananchi wa mkoa huo na mikoa ya kanda ya ziwa kwa kupata elimu ya jinsi ya kutumia barabara ili kupunguza ajali.

Mhe. Majaliwa amewataka wananchi wote kufuata sheria kanuni na miongozo ya kutumia barabara ili kupunguza ajali kwani Takwimu za ajali barabarani zilizofikishwa kwenye vyombo vya usalama na kutolewa taarifa  na jeshi la polisi  kwa miaka mitatu  iliyopita kuanzia Januari mwaka 2020 hadi Desemba, 2022  zilikuwa ni 5132 ziligharimu maisha ya watu 4060 na kusababisha majeruhi na walemavu 6427.


Aidha Mhe. Majaliwa ametoa jumla ya maagizo 13 kwa  Baraza la Taifa la Usalama Barabarani ili kupunguza au kumaliza changamoto ya ajali za barabarani ikiwemo kuharakisha  mchakato wa mapendekezo ya marekebisho ya sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuwa na sheria bora isiyoacha mwanya kwa watumiaji wote wa barabara wanaotembeza vyombo bila kuzingatia sheria, kufuatilia kuanzishwa kwa mfumo wa kuweka alama kwenye barabara na leseni za udereva ili kuwabaini madereva wanaokiuka sheria na iwe rahisi kuwachukulia hatua.

 “Pia Baraza litekeleze kwa ukamilifu maagizo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoyatoa kwenye maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani mwaka jana 2022 yaliyofanyika jijini Arusha kuhusu kuimarisha ukaguzi wa magari kwa kushirikisha sekta binafsi badala ya utaratibu wa sasa unaoshirikisha jeshi la polisi peke yake kukagua magari  maana magari ni mengi,”amesema Mhe. Majaliwa na kuongeza.

“Jeshi la polisi Tanzania liharakishe ufungaji wa mifumo ya  kielektroniki itakayokuwa inabaini makosa mbalimbali ambayo inasaidia kulinda mwenendo wa madereva wasiokuwa na maadili na pia itarahisisha ufanyaji kazi maana itatoa taarifa ni dereva yupi anayeendesha vyombo vya moto akiwa amelewa ,”amesisitiza Mhe. Majaliwa.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima amelishukuru Baraza la Taifa la Usalama Barabarani kwa kuuchagua mkoa huo kuwa mwenyeji wa maadhimisho ya wiki ya nenda kwa usalama barabarani  na kubainisha kwamba   watakuwa kinara wa kuheshimu  sheria, kanuni na taratibu  za Barabarani ambapo pia alimuomba Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa kupeleka maadhimisho hayo mwakani mkoani humo.

Maadhimisho ya wiki ya nenda kwa Usalama Barabarani mwaka huu 2023, yanaongozwa na Kauli Mbiu Isemayo 'Tanzania bila ajali inawezekana -Timiza wajibu wako.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.