• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Dkt.Mpango ahitimisha ziara Mkoani Mwanza kwa ahadi ya kutatua kero za wananchi Ukerewe

Posted on: November 25th, 2022


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Philip Mpango ameiagiza Wizara ya Maji kuondoa kero ya Upatikanaji Maji kwa wananchi wa Wilaya ya Ukerewe kwa kusimamia kwa ukaribu mradi Mkubwa wa Maji Kaziranganda wenye thamani ya Bilioni 7 na miradi mingine 11  inayotekelezwa ili ikamilike kwa ufanisi.

Dkt. Mpango ametoa agizo hilo leo (Novemba 25, 2022) wilayani humo wakati akihutubia wananchi wa Wilaya hiyo kwenye viwanja vya Getrude Mongela wakati akihitimisha ziara yake ya kikazi ya Siku nne Mkoani Mwanza.

Aidha, amemuagiza Mhe. Silinde kukagua mwenendo wa Uendeshaji wa Halmashauri ya Ukerewe kwani umekua na malalamiko mengi ya ubadhirifu. "Fedha za Miradi zitumike ipasavyo, nataka wanaodokoa wachukuliwe hatua zinazostahili na wakiwashinda waleteni kwangu mutaona nitakachowafanya" Amesisitiza Dkt. Mpango.

Vilevile, ameiagiza wizara ya Ujenzi kuanza Ujenzi wa Barabara ya Nansio, Kibara, Bunda na daraja la  Kisorya kwenye mwaka wa fedha ujao kwani ufanisi kwa ajili ya Ujenzi huo ulishafanyika na amemtaka Waziri wa Afya kuchunguza Ujenzi wa Hospitali ya Nansio iliyopelekewa Bilioni 3 na kudaiwa kuhujumiwa hatua kali zichukuliwe kwa wahusika.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Meja  Jenerali Suleiman Mzee (Mkuu wa Mkoa Mara) amemshukuru Mhe. Makamu wa Rais kwa ziara yake Mkoani Mwanza na amemuahidi kuyafanyia kazi maagizo yote aliyoyatoa kwa viongozi Mkoani humo.

Naibu waziri wa Maji, Mhe. Maryprisca Mahundi amesema wilaya ya Ukerewe inapata huduma a maji kwa asilimia 56 ya mahitaji ya wananchi wake na kwamba wizara hiyo itaendelea kutekeleza miradi ya maji kwa ufanisi mkubwa na hasa kurekebisha mfumo wa uendeshaji wa mradi mkubwa wa Maji wa Bilioni 7 na miradi yote 11 midogo inayoendelea kutekelezwa kwa zaidi ya Bilioni 16.

Akizungumzia suala la kuanzishwa kwa Mji mdogo wa Nansio, Naibu Waziri TAMISEMl, David Silinde amesema jukumu hilo hufanywa na Halmashauri Mama na kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina mapato duni ambayo hayawezi kuendesha mamlaka hiyo Mpya na kwamba kuna taratibu zinaendelea ili kupata ufumbuzi wa suala hilo.

Aidha, amewapongeza viongozi wa Halmashauri hiyo kwa kujenga Miundombinu ya madarasa hasa kwenye shule za kata zote ambapo suala hilo litasaidia kuwezesha wananfunzi kujiunga kidato cha kwanza wote wakltakaofaulu kutokana na uwepo wa Miundombinu ya kutosha.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Mhe. Reuben Sixbeth amesema kuwa Ukerewe imetekelwza Ilani kwa zaidi ya asilimia 60 kwa kutekeleza Miradi mbalimbali na akatumia wasaa huo kuitaka Kamati ya Siasa Wilaya hiyo kufuatilia kwa kina Miradi wa Maji yenye thamani ya Bilioni 7 ambayo inasuasua na Ujenzi wa Hospitali ya wilaya ambayo pamoja na uwepo wa fedha bado haiendi vema.

Mbunge wa Jimbo la Ukerewe Mhe. Joseph Mkundi ameishukuru Serikali kwa kuwaletea wananchi wa Jimbo hilo fedha za kutekeleza miradi Mbalimbali ya Maji, Elimu, Kilimo, Nishato ya Umeme, Barabara na Afya na kwa upekee ameshukuru kupata Pampu mbili mpya kwenye mradi mkubwa wa maji ambao sasa utaweza kuzalisha maji ya kutoshaleleza wananchi.

"Juzi mmetusaidia tani 300 kwa ajili kwa ajili ya kuwasaidia wananchi, tunashukuru sana kwa jambo hili ila tunaomba jambo moja nyeti la kujengewa ujenzi wa Barabara ya Kisorya kuja Nansio kwani ni sehemu muhimu sana kwa wananchi wa Ukerewe." Mhe. Mkundi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

    June 17, 2025
  • RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

    June 17, 2025
  • RC MTANDA ATOA MIEZI 2 KWA MANISPAA ILEMELA KUTENGENEZA MAGARI YASIYOTEMBEA

    June 17, 2025
  • RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.