• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

HALMASHAURI ZISIZOFANYA VIZURI MPANGO WA LISHE ZIANDIKIWE BARUA KALI: RAS BALANDYA

Posted on: March 5th, 2024

HALMASHAURI ZISIZOFANYA VIZURI MPANGO WA LISHE ZIANDIKIWE BARUA KALI: RAS BALANDYA


*Asema ukosefu wa Lishe unachangia kushuka kwa ufaulu shuleni*


*Ahimiza Halmashauri zote kutii agizo la Mpango wa lishe*


*Kwimba kinara wa chakula shuleni*


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana ameagiza Halmashauri zilizolega lega kutekeleza mpango wa lishe shuleni zichukuliwe hatua ya kuandikiwa barua kali.

Akizungumza leo Machi 05, 2024, Balandya amesema mwanafunzi anaposhinda bila kula shuleni ufuatiliaji wa masomo unashuka na hatimaye kufanya vibaya katika masomo yake.

"Nawasihi sana viongozi wenzangu hili suala la lishe tukalisimamie vizuri, Serikali imeboresha miundombinu ya elimu ni lazima iende pamoja na ufaulu wa kiwango," amesisitiza Mtendaji huyo wa Mkoa wakati wa kikao kazi cha Kamati ya Lishe.

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Thomas Rutachunzibwa amebainisha kuwa bado kunahitajika mkazo wa kuelimishana licha ya ukweli hali za kimaisha zinachangia mtoto chini ya miaka 5 kukosa lishe bora.

"Wakina mama walio wengi ndiyo wazalishaji wa chakula cha familia, kuelemewa na shughuli za kusaka kipato anajikuta mtoto hamnyonyeshi inavyotakiwa na tutambue maziwa ya mama yana virutubisho vingi," Mganga Mkuu wa Mkoa.

Afisa Lishe wa Mkoa Sophia Lugome, amesema jumla ya watoto 85,683 wa miezi 6-59 wamepatiwa matone ya Vitamin A na watumishi 532 wamejengewa uwezo kuhusiana na elimu ya Lishe.

"Ulaji wa chakula shuleni ni 75.2% kwa Mkoa mzima hapo bado kuna changamoto kwani inaonesha Halmashauri nyingi bado zina suasua katika uhamasishaji wazazi kuchangia mlo kwa wanafunzi," Afisa Lishe.

Amesema ni wilaya ya Kwimba pekee ambayo inaendelea kufanya vizuri suala la wanafunzi kula shuleni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MAKUZI YA AWALI YA MTOTO MSINGI WA UJENZI WA TAIFA IMARA - RAS BALANDYA

    May 16, 2025
  • RC MTANDA AWAKARIBISHA MWANZA WANAFUNZI KUTOKA UGANDA

    May 15, 2025
  • RC MTANDA AKOSHWA NA BONANZA LA USHIRIKA NA MABENKI

    May 14, 2025
  • RAS MWANZA ATAKA UHAMASISHAJI CHAKULA CHENYE LISHE KUONGEZEKA SHULENI

    May 13, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.