• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Kituo cha Afya Igalla-Ukerewe kuanza kutoa huduma mwakani

Posted on: November 25th, 2022


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango  ameagiza ifikapo mwishoni mwa mwezi februari 2023 kuanza kutolewa kwa huduma za Afya kwenye Kituo cha Afya Igalla wilayani Ukerewe ili wananchi wa eneo hilo wapate huduma muhimu ya afya jirani na makazi yao.

Dkt. Mpango ametoa agizo hilo mapema leo Wilayani Ukerewe alipofika kukagua ujenzi wa Kituo hicho kilichofikia zaidi ya Asilimia 95 ya ujenzi huku kikigharimu zaidi ya Milioni 492 ambapo kinatarajiwa kuwanufaisha wananchi zaidi ya elfu 17,000 kutoka kwenye kata ya Igalla  na kata za jirani za Bwiro, Mukituntu na Nduluma.

Akizungumza na wananchi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mpango amesema serikali itaendelea kufanya jitihada za kila namna kuajiri watumishi wa Afya kila wakati ili wakidhi mahitaji na amewataka wananchi kutunza amani ili wawe na uhuru wa kufanya kazi zitakazowainua kiuchumi.

Vilevile, ametoa rai kwa wananchi kuendelea kufanya kazi kwa bidii ikiwa ni pamoja na kutumia mvua vema katika kilimo ili wapate vyakula kwa ajili ya mahitaji yao na wawe na tabia ya kuweka akiba pamoja na kutunza Mazingira kwa kupanda miti kama sehemu ya Maisha yao.

Hata hivyo, amekemea tabia ya kuwapa mimba wanafunzi katika umri mdogo huku akibainisha kuwa matatizo kama ugonjwa wa Fistula yanatokana na uzazi katika umri mdogo na badala yake amewataka wazazi kuhakikisha watoto wao wanasoma kwa bidii.

Naibu Waziri wa TAMISEMl, Mhe. David Silinde amemshukuru Makamu wa Rais kwa kufika kwenye ujenzi huo ambao umetekelezwa vema kwa kutumia fedha za Mapato ya ndani kutokana na maelekezo ya viongozi wakuu wa nchi kupitia Wizara hiyo.

Kuhusu Vifaa Tiba, Mhe. Silinde amesema Vifaa Tiba vitaletwa kwenye kituo hicho cha Afya mara moja ili wananchi waweze kupata huduma za afya zilizo bora na kwa wakati tofauti na siku za nyuma ambapo walilazimika kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hizo.

Naye, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Ukerewe Emmanuel Sherembi amesema tayari Halmashauri hiyo imepokea watumishi 58 wapya na kwamba kwenye kituo hicho watapata watumishi akiwemo Mganga kwa kipaumbele ili huduma zianze mara moja.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Dkt. Getela Nyangi amesema Ujenzi wa Kituo cha Afya Igalla utasaidia kupunguza gharama za usafiri kwa wananchi waliokua wakifuata siku huduma za Afya, Kupunguza msongamano katika Hospitali ya Wilaya pamoja na kupunguza idadi ya Vifo kutokana kupata huduma hiyo jirani.

Aidha, Dkt. Nyangi amewasilisha Ombi  Maalumu kwa Mhe. Makamu wa Rais la  kununuliwa vifaa tiba vya kisasa, Jenereta,  Jengo la kufulia pamoja na wodi ya wanaume ili kukamilisha huduma zote kwenye kituo hicho kwani kwa upande wa majengo yanatarajiwa kukamilika ifikapo Disemba 20, 2022.

Awali, Dkt. Philip Mpango alikagua na kufungua Mradi wa Shule ya Sekondari ya Ukerewe iliyojengwa kwa Tshs Bilioni 1.1 kutoka Serikali kuu ambapo amewapongeza viongozi wa Wilaya hiyo kwa Utekelezaji wa mradi huo muhimu kwa maendeleo ya Sekta ya Elimu na akawataka kukamilisha Ujenzi wa Maabara ya fizikia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.