• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MAMLAKA ZA USIMAMIZI HUDUMA ZA MAJI NI NYENZO YA HUDUMA BORA- RAS BALANDYA

Posted on: September 2nd, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya amezipongeza na kutoa wito kwa Mamlaka za usimamizi wa huduma za Maji nchini kuendelea kuzijengea uwezo taasisi za Maji hususani katika kugawa rasilimali, kukabiliana na dharura, na kuhakikisha uendelevu wa kifedha na kiutendaji.

Bwana Balandya amesema hayo leo tarehe 02 Septemba, 2025 wakati akifungua warsha ya mafunzo kuhusu usimamizi wa mashirika ya maji yaliyoandaliwa kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Maji, taasisi ya IHE Delft kutoka Uholanzi, Hamburg Wasser kutoka Ujerumani na GIZ pamoja na mashirika ya maji nchini Tanzania.

Aidha, amezipongeza mamlaka hizo kwa kuwa nyenzo ya mafunzo ya vitendo katika kusimamia huduma za maji kwa ufanisi mathalani katika eneo la uandaaji wa mipango mikakati ya muda mrefu na mfupi katika kuhakikisha huduma za maji kwa jamii zinakua bora siku hadi siku.

“Usimamizi wa huduma za maji ni zana madhubuti ya kujifunza jinsi ya kusawazisha mahitaji ya sasa na mipango ya muda mrefu katika utoaji wa huduma za maji kwa wananchi,” amesema RAS Balandya.

Kadhalika, amewasisitiza washiriki wa mafunzo hayo kuhudhuria kikamilifu na kujibidiisha katika kupata ujuzi mpya utakaofundishwa hususani masuala ya teknolojia za kisasa kwenye maji ili watakaporudi katika mamlaka zao wakasaidie kuboresha maisha ya wananchi.

“Mnapoanza safari ya warsha nawahimiza mshiriki kikamiliífu, muwe wazi, mshirikiane na mjitahidi zaidi kutoa changamoto kwa uhuru na mtumie nafasi hii kikamilifu ili mkaboreshe maisha ya mamilioni ya watanzania wanaotegemea huduma bora za maji kutoka kwetu.” Amesema Ndg. Balandya.

Naye, Mkurugenzi  wa ufatiliaji na uwekezaji kutoka Wizara ya maji Bi. Diana Kimario amesema matokeo ya mafunzo hayo yanaweza kusaidia kuandaa kukabiliana na changamoto pamoja na uwajibikaji kwa wananchi wanaotumia huduma za maji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA MWANZA KUCHANGAMKIA DIRISHA LA UWEZESHAJI

    September 03, 2025
  • RC MTANDA AWAASA TCCIA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZINAZOHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI

    September 02, 2025
  • WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO MWANZA WAHIMIZWA KUIMARISHA NIDHAMU ILI KUKUA KIUENDELEVU

    September 02, 2025
  • MAMLAKA ZA USIMAMIZI HUDUMA ZA MAJI NI NYENZO YA HUDUMA BORA- RAS BALANDYA

    September 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.