• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI MWANZA KUWA WABUNIFU UHABARISHAJI UMMA

Posted on: July 19th, 2024

MSEMAJI MKUU WA SERIKALI AWATAKA MAAFISA HABARI MWANZA KUWA WABUNIFU UHABARISHAJI UMMA


Mkurugenzi wa Idara ya Habari Maelezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bwana Thobias Makoba amewataka Maafisa Habari wa Serikali Mkoani Mwanza kubuni habari mpya za kimkakati zenye kuitangaza miradi ya maendeleo ya Serikali badala ya kusubiri matukio.

Bwana Makoba ameyasema hayo leo Julai 19, 2024 wakati alipokua akizungumza na Maafisa Mawasiliano kutoka Tawala za Mikoa na Serikali za mitaa, Taasisi, Mashirika na Makampuni  mbalimbali ya Serikali Mkoa wa Mwanza katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo.

Bwana Makoba amesema anatamani kuona Maafisa hao wakiwa wabunifu zaidi katika kuhakikisha wanauhabarisha umma kwa namna ambayo siyo ya kutegemea habari kutoka kwa viongozi tu bali  watumie mbinu mbalimbali ili kuonesha utofauti wa utendaji wa sasa na siku za nyuma.

"Na hapa Mwanza ninajua kuna miradi mbalimbali ya kimkakati kama vile ujenzi wa reli ya SGR hivyo tusisubiri ijitokeze  dosari ukimbilie kutoa taarifa ya ufafanuzi , ni wakati sasa wa kubadili  namna ya utoaji wa taarifa zetu". Amesisitiza Makoba.

Aidha, amesema umekua ni utaratibu wake kukutana na Maafisa Mawasiliano kila mahali aendapo lengo likiwa ni kujitambulisha lakini pia kusikiliza na kuchukua maoni, mawazo na mapendekezo mbalimbali ambayo yatasaidia kuboresha utendaji kazi.

"Kuwa msemaji mkuu siyo kwamba unajua kila kitu, tunategemeana katika kuhabarisha kwani Serikali ni moja, " amefafanua Makoba.

Awali, Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amesema Mkoa wa Mwanza ni Mkoa wa kimkakati kwa kuwa ndiyo lango kuu kwa kanda ya ziwa na ndiyo kitovu cha uchumi hivyo Maafisa Habari wanategemewa kwenye uhabarishaji na Serikali inawapa ushirikiano mzuri.

Naye Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali (RS Mwanza) Bw. Paulo Zahoro amesema hali ya uhabarishaji kwa Mkoa wa Mwanza ni nzuri hata kufikia hatua ya kushinda nafasi ya pili na kupata Kikombe na Cheti cha ushindi kutoka kwa Waziri wa Habari Mhe. Nape Nnauye kwenye Kongamano la Habari lililofanyika jijini Dar es Salaam Juni mwaka huu.

Maafisa Mawasiliano nao wamemshukuru Msemaji Mkuu wa Serikali kwa kutambua umuhimu wao ambapo wamemuahidi kutimiza wajibu wao kwa kuhabarisha jamii juu ya mambo mbalimbali yanayotekelezwa na Serikali.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.