• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

PPRA YAWANOA WARATIBU WA WASH MFUMO WA NeST

Posted on: February 6th, 2025

PPRA YAWANOA WARATIBU WA WASH MFUMO WA NeST


Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma-PPRA inaendesha mafunzo juu ya Mfumo wa Usimamizi wa Ununuzi wa Umma (NeST) kwa Maafisa ununuzi, Waratibi na Wasimamizi wa mradi  wa Programu za Uendelevu wa Usambazaji wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (WASH) ngazi ya Mkoa na Halmashauri Mkoani Mwanza.

Mafunzo hayo yaliyoanza rasmi leo Februari 06, 2025 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza yamefunguliwa na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Ndugu Kusirie Swai na amewataka washiriki hao kufanya manunuzi yote kupitia Mfumo wa NeST.

Ndg. Swai amesema Mkoa wa Mwanza ni miongoni mwa Mikoa inayotekeleza programu ya WASH ambapo utekelezaji wa Programu hiyo unahusisha kufanya manunuzi mbambali kupitia Mfumo wa NeST hivyo ni muhimu kwa wahusika wa manunuzi kuwa na uelewa wa kutosha kuhusu matumizi ya mfumo huo.

“Ndugu Washiriki wa mafunzo, kutokana na umuhimu wa utekelezaji wa programu, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa imeandaa mafunzo haya ili kuwajengea uwezo wafawidhi wa vituo vitakavyotekeleza mradi kwa mwaka 2024/2025”. Ndugu Swai.

Aidha, amesema mafunzo hayo ni muhimu kwao na wanapaswa kuyatilia maanani ili iwasaidie katika kuwezesha utekelezaji wa programu kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu katika ununuzi wa umma.

Kwa upande wake Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amewapongeza wadau hao kwa kazi nzuri wanayofanya katika kusambaza maji na huduma ya usafi wa mazingira Mkoani humo na akatoa wito kwao kuhakikisha wanakuwa makini ili wakayatumie mafunzo hayo katika kufanya manunuzi kwa njia ya kielektroniki bila kukwama.

Aidha, Mganga Mkuu wamesisitiza umuhimu wa kufuata miongozo ya utekelezaji wa kazi hizo ili kuhakikisha miradi kama vyoo, vichomea taka, matenki ya maji na vinginevyo viweze kukamilika kwa wakati na kwa ubora unaokusudiwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.