• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

PROF. SHEMDOE ATAKA KUWEKWA MKAKATI WA KIMATAIFA KUDHIBITI UVUVI HARAMU ZIWA VICTORIA

Posted on: August 26th, 2024

PROF. SHEMDOE ATAKA KUWEKWA MKAKATI WA KIMATAIFA KUDHIBITI UVUVI HARAMU ZIWA VICTORIA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe ametoa rai kwa Mataifa ya Kenya, Uganda na Tanzania, kufanya doria ya pamoja katika ziwa victoria, ili kukomesha uvuvi haramu na biashara ya mazao ya uvuvi, inayokiuka taratibu za kisheria ndani ya ziwa hilo.

Akifungua mkutano leo Agosti 26, 2024 wa kuhamasisha wadau wa uvuvi kudhibiti uvuvi haramu na biashara haramu ya mazao ya uvuvi ziwa victoria kwenye ukumbi wa mikutano Nyakahoja, Katibu Mkuu huyo amesema ziwa Viktoria linamchango wa asilimia 67% katika sekta ya uvuvi nchini, likiwa limeshuka kwa asilimia 17% kutoka 85%, likiwa na wavuvi 100,002, huku wanufaika wa moja kwa moja wa biashara ya mazao ya uvuvi wakiwa zaidi ya laki mbili.

"Serikali kwa kutambua mchango wa sekta hii inaendelea kuiboresha ikiwa pamoja na kutoa boti za kisasa na ukopeshaji bila riba kwa makundi maalum ya Ufugaji wa samaki wa vizimba".

Lakini Pamoja na mchango huo, kikwazo kikubwa kinacholikabili ziwa hili ni uvuvi haramu unaoangamiza mazalia ya rasilimali zilizopo ziwani humo". Amesisitiza Katibu Mkuu.

Aidha amewataka wadau wa sekta ya uvuvi kukaa na kuja na mikakati endelevu ya kimataifa ya kukomesha hali hiyo na kuiwasilisha Serikalini ili ifanyiwe maboresho mazuri na ziwa liendelee kuwa na tija kwa wananchi wa Mwanza na nchi jirani zinazozungukwa na ziwa hilo.

Kadhalika ameendela kwa kusema mradi wa uvuvi wa vizimba uliozinduliwa na Mhe. Rais mapema mwaka huu umekuwa na matokeo chanya na umeendelea kufanya vizuri, ambapo amesema wametoa boti 160 nchi nzima na 151 zimefanya vizuri.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohamed Sheikh, amesema hali ya uvuvi haramu imechangia uvunaji wa tani za samaki kushuka katika ziwa victoria, ukihusisha samaki aina ya sangara, dagaa, mabondo na mauzo kuporomoka.

"Wizara inakuja na mkakati wa kisasa wa kupambana na hali hiyo ukiwemo utumiaji wa ndege nyuki ili kuwabaini wanaojihusisha na uvuvi haramu na vifaa maalum vya ufuatiliaji". Amesema Prof. Sheikh

Akitoa Salamu za Mkoa kumuwakilisha Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza, Katibu Tawala Msaidizi, Uchumi na Uzalishaji, Bw. Emil Kasagara amesema viwanda vingi kwa sasa vinashindwa kujiendesha kwa ufanisi na vingine vikiyumba kutokana na upungufu wa rasilimali ziwa unaochangiwa na uvuvi haramu.

"Tumekuwa na vikao mbalimbali na wadau wa sekta hii kwa lengo la kuelimishana na kuhakikisha ziwa linaendelea kuwa kitega uchumi muhimu kwa wananchi" Kasagara.

Mkutano huo umewashirikisha Maafisa uvuvi kutoka Mwanza, Mikoa ya jirani na sekta binafsi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.