• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA AHIMIZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO H/ZA BUCHOSA NA SENGEREMA

Posted on: June 26th, 2024

RAS BALANDYA AHIMIZA KASI YA UKUSANYAJI MAPATO H/ZA BUCHOSA NA SENGEREMA


Halmashauri za Buchosa na Sengerema zimehimizwa kuwa na kasi ya ukusanyaji wa mapato ya ndani ili wazidi kuboresha huduma kwa wananchi na kupangilia mipango ya maendeleo kwa uhakika.

Rai hiyo imetolewa leo Juni 26,2024 kwa nyakati tofauti kwenye halmashauri hizo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw Balandya Elikana wakati wa vikao vya Baraza la Madiwani kujadili  hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali,CAG za mwaka wa Fedha 2022-23,amesema Halmashauri hizo zikiweka mkakati mzuri wa ukusanyaji mapato tija ya maendeleo kwa wananchi itazidi kuimarika.

"Nimesikia mlivyovuka malengo yenu ya ukusanyaji mapato hapa Buchosa kwa kuvuka zaidi ya asilimia 100,hongereni sana sasa ongezeni bidii kuanzia sasa ili muweze kuwa na miradi mingi ya kuwaletea maendeleo wananchi,"Balandya

Mtendaji huyo wa Mkoa amewataka pia Madiwani wa Halmashauri hiyo kusimamia vyema miradi ya maendeleo na kutoruhusi hoja za CAG kujirudia.

"Halmashauri ya Buchosa katika ukaguzi wa Hesabu za CAG mwaka 2022-23 walikuwa na hoja 6,tano za zamani na moja ya 2022-23 ambayo ipo katika utekelezaji,"Laban Kilulu,Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu Serikali

Akiwa kwenye halmashauri ya Sengerema iliyofikisha asilimia 86 ya mapato yake ya ndani Balandya ametoa maagizo ya kuhakikisha hoja zote zikamilishwe kwa wakati.

"Hesabu za CAG zinaonesha mmepata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo na mlikuwa na hoja 17 na 16 mmezikamilisha na kubakiza 4 za nyuma ambazo nataka zikamilishwe,"Mtendaji wa Mkoa

Kuhusu madeni ya wazabuni ya zaidi ya milioni 400 amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Sengerema kuongeza bajeti ya kuwalipa ili waweze kumudu shughuli zao

"Haiwezekani Mkurugenzi ukatenga milioni 50 ya kuwalipa wazabuni ni dhahiri utawapa umasikini kwa kushindwa kuwalipa kwa muda mrefu",amesisitiza Balandya

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe.Senyi Ngaga amebainisha maagizo yote yaliyotolewa watayafanyia kazi na hasa ukusanyaji mapato ya ndani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.