• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS BALANDYA AMEWATAKA WAHITIMU IFM KUWA MABALOZI WAZURI WA CHUO CHAO

Posted on: December 6th, 2025

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Bw. Balandya Elikana amewataka wahitimu kuwa mabalozi wazuri wa chuo chao kwa kufuata waliyofundishwa darasani na kuzingatia weledi, ujuzi na nidhamu haswa katika jamii zinazowazunguka.

Amesema hayo kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza katika mahafali ya 51 ya chuo cha usimamizi wa fedha (IFM) katika kampasi za Mwanza, Simiyu na Geita yaliyofanyika leo Disemba 6, 2025 katika ukumbi wa Rockcity mall manispaa ya Ilemela.

Ameendelea kwa kuwataka wahitimu hao kutumia mradi wa elimu ya juu wa mageuzi ya kiuchumi (HEET) wenye lengo la kukuza elimu ya juu kama chachu ya kuleta uchumi mpya wa Tanzania.

Kadhalika amewaasa wahadhiri wa IFM kuendelea kuwafundisha vyema wanafunzi wanaoendelea na kwa juhudi kubwa ili kuendelea kuboresha mitaala na kuendana na mahitaji mbalimbali.

Aidha ametoa wito kwa uongozi wa chuo cha IFM kuendelea kutoa elimu yenye ubora na kuendelea kuzalisha wataalamu huku akisisitiza kuongeza kozi za kufundisha katika kampasi za kanda ya ziwa kwani zitaenda kuongeza wataalamu na kupunguza changamoto mbali mbali katika jamii.

Awali akisoma risala Mkuu wa chuo cha IFM Prof. Josephat Lotto ameishukuru serikali kwa misaada ya fedha na miongozo ambayo imesaidia katika kuhakikisha wanaziendeleza kampasi za Mwanza, Geita na Simiyu lakini pia kwa kukipatia chuo nafasi za kuajiri watumishi mbalimbali.

Naye mwenyekiti wa baraza la uongozi wa chuo Prof. Emmanuel Mjema ameiomba serikali iweze kuwasaidia kuongeza nguvu katika ukuzaji wa rasilimali watu huku akisema kuwa ujenzi wa chuo na mabweni katika kata ya Kisesa unaendelea kwa kiwango cha kuridhisha, na amewasihi wahitimu waweze kujiendeleza kielimu ili kuendelea kukuza utambuzi na uelewa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA AMEWATAKA WAHITIMU IFM KUWA MABALOZI WAZURI WA CHUO CHAO

    December 06, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZINAZOPATIKANA

    December 06, 2025
  • SERIKALI YATENGA FEDHA KUKAMILISHA MIRADI YA MAENDELEO MWANZA - DKT. NCHEMBA

    December 05, 2025
  • DKT. NCHEMBA ATOA POLE KWA WANANCHI WALIOHARIBIWA MALI KUTOKANA NA VURUGU MKOANI MWANZA

    December 05, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.