• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RAS MWANZA ATOA WITO KWA WADAU WA AFYA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUSAIDIA SEKTA HIYO

Posted on: February 7th, 2025

RAS MWANZA ATOA WITO KWA WADAU WA AFYA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUSAIDIA SEKTA HIYO


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza ndugu Balandya Elikana ameipongeza Idara ya Afya Mkoani humo kwa ufanisi kwenye kazi kwa kushirikiana na wadau jambo linalofanya Mwanza iendelee kuwa salama wakati wote pamoja na uwepo wa hatari ya magonjwa ya mlipuko.

Ametoa pongezi hizo leo tarehe 07 februari, 2025 wakati akifungua kikao cha Wadau wa Afya kilichoketi kwenye Ukumbi mdogo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa madhumuni ya kukumbushana wajibu katika kuhudumia jamii ili iendelee kuwa salama.

Aidha, amebainisha kuwa Mkoa wa Mwanza umejipanga kukabiliana na magonjwa ya Mlipuko kama Marburg pamoja na kuendelea kutoa huduma bora za afya kwa kushirikiana na wahisani wa ndani kutokana na kujitoa kwa baadhi ya mataifa tajiri.

Amesema, Mwanza imeshaandaa kikosi kazi cha watumishi wa afya zaidi ya 264 ambao wamepewa mafunzo maalumu ya mapambano ya ugonjwa huo na jinsi ya kumhudumia mgonjwa atakayeambukizwa na akatoa wito kwa wadau kuunga mkono juhudi hizo kwa rasilimali zozote zitakapohitajika.

Halikadhalika, ametoa wito kwa wadau kushirikiana na serikali katika kuhudumia watumishi zaidi ya 600 waliokua kwenye ufadhili wa mashirika wahisani kutoka nje ili huduma za msingi zisikwame kwa kutumia rasilimali zilizopo.

Naye, Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amebainisha kuwa idara ya Afya mkoani humo wameamua kukutana na Wadau pamoja na mambo mengine ili kupitia maandalizi ya bajeti 2025/2026 na kuandaa mpango kazi wa mwendelezo wa kazi za afya baada ya baadhi ya wahisani wa nje kujitoa kwenye ufadhili.

Kaimu mratibu wa magonjwa ya milipuko Dkt. Gabriel Mashauri amesema Marburg ni ugonjwa wa mlipuko unaosababishwa na virusi vya Marburg na unaambukizwa kwa haraka kupitia njia ya damu, mate, mkojo, jasho, choo kikubwa, matapishi, maji ya uzazi na hata kugusana na dalili zake ni kutokwa damu mwilini.

Amefafanua kuwa wafanyakazi wa Afya wapo kwenye hatari zaidi ya kuambukizwa  na uwezekano wa kifo hutofautiana kati ya 24% hadi 88% hivyo ni ugonjwa hatari unaosababisha vifo kwa haraka hivyo basi watu wanapaswa kuelimishwa kutochangia nguo au vitu vyenye ncha kali.

Aidha, Dkt. Mashauri amezitaja dalili za mtu aliyepata na maambukizi hayo kuwa ni pamoja na  kuumwa kichwa, homa, maumivu ya misuli, mwili kuishiwa nguvu, vidonda vya koo, vipele vya ngozi, maumivu ya tumbo, kuharisha (damu), kutapika damu na kutokwa damu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.