• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Makalla akabidhiwa rasmi Ofisi,amshukuru Rais Samia kwa kumuamini na kuahidi kuchapa kazi kwa uaminifu na bidii

Posted on: May 28th, 2023

*RC Makalla akabidhiwa rasmi Ofisi,amshukuru Rais Samia kwa kumuamini na kuahidi kuchapa kazi kwa uaminifu na bidii*


 *Awaahidi wana Mwanza kasi ya Maendeleo kwa kushinda Site na *kusikiliza kero zao*


 *Kulivalia njuga tatizo la Maji*


 *Apania Mwanza kuwa na timu ya Ligi Kuu ya NBC*



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Amos Makalla amekabidhiwa rasmi Ofisi kutoka kwa mtangulizi wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe.Adam Malima na kuahidi kuyatekeleza kwa bidii na uaminifu matarajio yote ya Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan ya kuwaletea maendeleo wananchi  na kuinua kwa ujumla uchumi wa Mkoa huo.

Akizungumza leo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na viongozi waandamizi wa Serikali, Taasisi na wawakilishi kutoka makundi mbalimbali,Mhe Makalla amesema anatambua amekuja kwenye Mkoa ambao unahitaji kuwa na kiongozi wa mfano katika  kuwatumikia wananchi na kuitekeleza kwa vitendo Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

"Mimi siyo mtu wa kukaa Ofisini,muda wote napenda kushinda Site huko ndiyo nitapata kujua ukweli wote wa kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi,nitaanza ziara ya kutembelea Wilaya zote kuanzia tarehe 31 2023",Amesisitiza CPA Makalla.

Aidha kuhusu kero ya maji kwa wananchi wa Mwanza hasa wanaoishi maeneo ya milimani na kwingineko,Mkuu huyo wa Mkoa ameahidi kulivalia njuga suala hilo kwani ana uzoefu wa kutosha alipokuwa Naibu Waziri wa Maji, hivyo ameomba ushirikiano wa dhati kutoka kwa Taasisi husika ili kumaliza kero hiyo.

Kuhusu miradi yote ya kimkakati iliyopo Mkoani humo Mhe.Makalla amebainisha ataitembelea na kuhakikisha inamalizika kwa wakati na kuwa na tija kwa wananchi.

"Ziara yangu nitakayoanza hivi karibuni nataka kuiona miradi yote iliyopo inatekelezeka kwa usahihi na wananchi wanapata maendeleo kwa haraka na nitawapa nafasi wananchi kusikiliza kero zao kama ilani ya CCM inavyotaka ",Mhe.Makalla

Mkuu huyo wa Mkoa wa Mwanza ambaye pia ni mkereketwa wa michezo amesema haoni sababu ya Mkoa huo kukosa timu ya kucheza Ligi kuu ya NBC kutokana na nguvu ya kiuchumi iliyonayo,hivyo atahakikisha anakusanya nguvu za Wadau ili kufanikisha malengo hayo.

Awali akisoma taarifa ya Mkoa ,Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Mhe.Adam Malima amesema bado Mkoa wa Mwanza unakabiliwa na Changamoto mbalimbali ikiwemo kero ya maji,uhaba wa fedha za kukamilisha huduma za jengo jipya la wagonjwa wa Saratani Bugando kutokana na wingi wa wagonjwa wanaotoka Kanda ya ziwa,uharibifu wa Mazingira,na ubadhilifu wa fedha za mikopo kwa makundi maalum kutoka kwenye Halmashauri.

"Mhe.Makalla nakuwachia mambo manne ambayo ni vyema ukaanza nayo,jengo la uwanja wa ndege bado halina ubora kama kweli tunahitaji kukuza soko la utalii,Mgodi wa Madini wa Nyazaga wapo katika hatua ya kuwalipa fidia wananchi umakini unahitajika katika zoezi hili,Zao la Pamba ambalo ni uti wa mgongo kwa Mkoa wa Mwanza bado halimnufaishi Mkulima,Wafugaji Mwanza wanafikia idadi ya 50,000 lakini bado mifugo yao haina tija licha ya Serikali kuwekeza fedha nyingi Sekta ya Kilimo na Mifugo",RC Malima.

Katika hafla hiyo fupi ya makabidhiano ya Ofisi imeambatana na utoaji wa zawadi mbalimbali alizokabidhiwa Mhe.Malima zikiwemo picha za matukio kadhaa aliyoshiriki akiwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, ikiwemo kampeni ya Mkoa huo ya upandaji miti Milioni 23.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.