• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awaaga Pamba FC,awataka watimize ndoto yake kuiona ikicheza Ligi Kuu ya NBC

Posted on: May 16th, 2023

*RC Malima awaaga wachezaji wa Pamba FC, awaasa kutokata tamaa*


Mkuu wa Mkoa wa Morogoro aliyehamishiwa akitokea Mwanza, Mhe. Adam Malima amewaaga wachezaji wa timu ya soka ya Pamba FC iliyopo ligi ya Championship na kuwataka kutokata tamaa katika michezo yao ijayo ya Mchujo kuwania kucheza ligi kuu ya NBC kwa msimu ujao.

Akizungumza na wachezaji na viongozi wa timu hiyo leo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mhe. Malima amesema anaamini bado Pamba ni timu bora yenye uwezo wa kucheza Ligi kuu cha msingi ni wachezaji waongeze bidii.

"Sina shaka na nyie nimewaona uwezo wenu uwanjani, naamini dawati lenu la ufundi litafanya mkazo eneo la umaliziaji ili muweze kufunga mabao mengi,"amesema Mhe.Malima.

Malima amewasihi kushinda mchezo ujao wa mchujo dhidi ya Mashujaa FC utakaopigwa kwenye Dimba la Lake Tanganyika Mei 21, 2023 Mkoani Kigoma ili kurahisisha kazi mpambano wa marudiano utakaorindima uwanja wa Nyamagana Mei 28 2023.

Aidha, katika hafla hiyo Mkuu huyo mpya wa Mkoa wa Morogoro amewakabidhi wachezaji jumla ya Shilingi Milioni 3 ahadi yake ya fedha Shs Milioni moja pamoja na fedha kutoka kwa mdhamini wao Kampuni ya vinywaji baridi ya Jambo Shs Milioni 2.

Akitoa neno la shukrani kwa moyo aliouonesha kwa kuipambania timu hiyo Mwenyekiti wa Chama cha soka Mkoani Mwanza MZFA,Vedasto Lufano amesema wataendelea kumkumbuka Mhe. Malima kwa vitendo  kuhakikisha wanafikia malengo yao ya kucheza ligi kuu ya NBC.

"Hatuna namna yoyote ya kukufurahisha zaidi ya kutimiza ndoto zako ukiwa hapa Mkoani Mwanza kuiona Pamba FC ikicheza Ligi kuu ya NBC, hilo nakuahidi tunalipambania". Lufano

Nahodha wa Pamba FC, Jerryson Tegete amesema licha ya kukosa nafasi ya kufuzu moja kwa moja na badala yake wameingia mchezo wa mchujo wamejipanga kuwapa faraja wana Mwanza kuiona timu hiyo ikicheza Ligi kuu.

"Mhe.Malima kwa ari uliyotupa licha ya kuhamishiwa Morogoro hii ndoto yako ya kuiona Pamba FC inacheza Ligi kuu, kwa niaba ya wenzangu tunakuahidi kuitimiza," Tegete.

Pamba FC imemaliza michuano ya Ligi ya Championship msimu huu ikiwa nafasi ya tatu na mtaji wa pointi 59,hivyo kwa kanuni za TFF italazimika kucheza mchezo wa mchujo na Mashujaa FC waliomaliza wakiwa nafasi ya nne na point 49 na mshindi wa jumla atamsubiri kumenyana na timu kutoka Ligi kuu ya NBC.

Timu ya soka ya Pamba FC maarufu kama TP LINDANDA, mara ya mwisho kucheza Ligi kuu ilikuwa msimu wa mwaka 2000-2001.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.