• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awataka Wamachinga kufanya biashara kwenye maeneo rasmi

Posted on: December 20th, 2022

*RC Malima awataka Wamachinga kufanya biashara kwenye maeneo rasmi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima ametoa rai kwa Wafanyabiasha wadogo (Machinga) Mkoani humo kufanya biashara zao kwenye maeneo rasmi ili kuweka mazingira ya miji kuwa nadhifu yatakayovutia wageni hata kusaidia ukuaji wa Sekta ya Utalii.

Mhe. Malima amesema hayo leo jumanne disemba 20, 2022 wakati wa Kikao cha Kamati ya Ushauri cha Mkoa kilichohudhuriwa na viongozi wa kundi hilo na akaongeza kuwa endapo watakuwa na changamoto kwenye shughuli zao wanapaswa kuwasilisha kwenye mamlaka husika kwa ajili ya utatuzi.

"Natamani kila mwananchi wa nchi hii ambaye anaishi Mkoani Mwanza astawi kiuchumi kama malengo ya Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan alivyojipambanua katika falsafa ya uongozi wake na katika kuyafikia haya ni lazima kila mmoja afuate taratibu za kisekta." Malima.

Vilevile, ametoa wito kwa Halmashauri Mkoani humo kuwa na mipango thabiti ya Ukusanyaji wa mapato ikienda sambamba na uwezeshi wa makundi yote ya Wafanyabiasha kwa kuhakikisha huduma zote za kijamii zinapatikana.

Hata hivyo, ametoa wito kwa Mamlaka ya Maji  na Usafi wa Mazingira Mjini Mwanza ( MWAUWASA), Wakala wa Maji Mijini na Vijijini (RUWASA) na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Sengerema (SEUWASA) kutekeleza miradi ya Maji kwa ufanisi ili kuongeza Mtandao wa huduma ya Maji kwa wananchi.

Halikadhalika, Mhe. Malima amewahimiza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kukamilisha Ujenzi wa Jengo la Kisasa la abiria kwenye uwanja wa Ndege wa Mwanza ili kuweka mazingira rafiki kwa wageni kufika ambapo amebainisha kuwa uwepo wa Miundombinu hiyo itasaidia kukuza sekta ya Utalii kwa wageni kutalii kwenye hifadhi za kanda ya Ziwa wakitumia uwanja huo.

Akiwasilisha taarifa ya Timu iliyoundwa na Mkuu wa Mkoa kufuatilia Ukarabati wa Kivuko cha MV Misungwi, Katibu wa Kamati hiyo Chagu Ng'homa amesema TEMESA na Songoro Marine waliingia Mikataba miwili ya ukarabati wa Kivuko cha MV Misungwi na kukamilisha kufikia Machi 20, 2023.

Kamati hiyo imebaini kuwa Mkandarasi anao uwezo wa kukamilisha ukarabati huo ndani ya muda kwani tayari ameshaagiza Injini Mpya na vifaa vingine nchini Korea ambavyo kwa pamoja vitawasili nchini ifikapo Januari 30, 2023 lakini imeshauri kuwe na ufuatiliaji wa karibu kwenye karakana hiyo ili kusukuma utekelezaji.

Kwa upande wa Sekta ya elimu Mkuu huyo wa Mkoa ametaka kuwepo na jitihada za makusudi za kuwepo na uwiano mzuri wa walimu hasa maeneo ya nje ya mji ambako wengi hawapendi kwenda kufanya kazi.

Amesema Serikali imeweka mazingira rafiki kwa walimu waweze kufanya kazi vizuri ikiwemo kuwapatia nyumba bora lakin bado idadi kubwa wamerundikana mjini.

"Mkoa wa Mwanza umepatiwa zaidi ya Shs Bilioni 19 kwa ajili ya ujenzi wa madarasa kwenye Halmashauri zote za Mkoa huu na tuna uhakika wanafunzi wote waliofaulu kwa kidato cha kwanza mwakani watasoma kwenye mazingira bora" Afisa Elimu Mkoa Martin Nkwabi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.