• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AUPOKEA MSAFARA WA BALOZI KUTOKA BURUNDI

Posted on: July 13th, 2024

RC MTANDA AUPOKEA MSAFARA WA BALOZI KUTOKA BURUNDI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Julai 13, 2024 ameupokea Ofisini kwake msafara wa Balozi wa Tanzania nchini Burundi Mhe. Balozi Gelasius Byakanwa pamoja na wanafunzi na walimu wa vyuo vikuu kutoka mjini Bujumbura nchini Burundi.

Ugeni huo umewasili Mkoani Mwanza kwa lengo la kutembelea miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akizungumza mara baada ya kuwapokea wageni hao Mhe. Matanda amesema Serikali ya Tanzania chini ya Mhe. Rais Samia itaendelea kushirikiana na Serikali ya Burundi chini ya Mhe. Rais Ndayishimiye.

Aidha, Mtanda amewataka vijana hao kuhakikisha wanalinda amani waliyonayo kwani madhara na athari za uharibifu wa amani hiyo tayari wanazijua, hivyo amewataka kuiendeleza amani waliyonayo kwa kutokukubali kutumika kuvunja amani yao.

"Ukishashiba amani unaanza kuwaza kuharibu amani, ni lazima tujenge utaratibu wa kuthamini amani, nchi kama Burundi mna uzoefu mkubwa wa amani ni nini". Mhe. Mtanda.

Ukiwa katika nchi yako huwezi kuona thamani ya nchi uliyonayo ila ukiwa ugenini ambapo ni uhamishoni ndio utakapoona thamani ya nchi yako, Warundi lazima mjivunie Urundi wenu kwa sababu ndio thamani yenu. Ameongeza Mhe. Mtanda.

Kadhalika, Mhe. Mtanda amewasihi Wanafunzi na walimu hao kuhakikisha wanendelea kudumisha umoja wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa kuidumisha na kuiendeleza lugha ya kiswahili ili pia kiweze kukidhi vigezo vya kutumika katika nyanja nzima ya teknolojia.

Naye Balozi wa Tanzania nchini Burundi , Mhe. Balozi Gelasius  Byakanwa amesema wao kama ubalozi waliamua kwa juhudi zote kuikuza na kuisambaza lugha ya kiswahili na wakaona waje na utaratibu wa kushindanisha wanafunzi wa vyuo vikuu katika uandishi wa insha mjini Bunjura, lengo likiwa ni kuhakikisha wanakikuza na kukiendeleza lugha adhimu ya kiswahili.

Aidha Mhe. Balozi Byakanwa amesema wako Mkoani Mwanza kujionea yale mazuri yaliyofanywa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo miradi mikubwa ya kimkakati kama vile mradi wa daraja la kigongo - Busisi, ujenzi wa Neli kubwa ya Mv. Mwanza Hapa  Kazi Tu.

"Nina imani hawa vijana watakua mabalozi wazuri wa lugha ya kiswahili na yale tuliyoyashuhudia hapa Mwanza na hawa wataleta watu wengi zaidi, lakini pia hawa tunaweza kuwaita wavuvi ambao watakwenda kuvua wengi zaidi waje kutalii Mkoani Mwanza".

Vijana hawa jana wameshuhudia kwa macho yao namna daraja lilivyojengwa juu ya maji, ujenzi wa Meli ya Mv. Mwanza Hapa Kazi Tu na wengine pia walikua hawajawahi kupanda hata meli hivyo wamepanda hapa Mwanza, nikuhakikishie RC, hawa watakwenda kuutangaza vyema Mkoa huu wa Mwanza. Ameongeza Mhe. Balozi Byakanwa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.