• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWAASA TCCIA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZINAZOHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI

Posted on: September 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa Chemba ya  wafanyabiashara nchini TCCIA kuzingatia sera za biashara na viwanda pia kuzingatia kilimo endelevu kinachotumia teknolojia zinazohimili mabadiliko ya tabianchi ili kuongeza tija katika kazi zao.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo jumanne tarehe 02 Septemba, 2025 wakati akifungua maonesho ya 20 ya Biashara ya Afrika Mashariki katika Uwanja wa Nyamagana.

Amesema kadri siku zinavyokwenda jamii imekua ikiongezeka na kusababisha uharibifu wa mazingira hivyo chemba hiyo ina wajibu wa kutoa elimu kwa jamii kufanya shughuli za Uvuvi, biashara na kilimo cha kisasa pasipo kuharibu mazingira ili kuwa na jamii endelevu.

Aidha, amesema kuwa Serikali inaendelea kuwahimiza na kuwawezesha Wafanyabiashara kuchangamkia fursa zilizopo katika soko la Afrika Mashariki katika Nchi za Kenya, Uganda, Congo, Tanzanıa, Kusini, Burundi, Rwanda na Sudan.

“Maonesho haya ni jukwaa la kuimarisha mahusiano ya kibiashara kwa kubadilishana ujuzi, uzoefu na mazingira ya biashara. Pia yanatoa fursa kwa kampuni za ndani kujifunza Mbinu za kukuza biashara ya nje kwa kutumia masoko ya kimataifa kama SADC, AFCFTA, India, AGOA na China” Mhe. Mtanda.

Rais wa Chemba ya Wafanyabiashara Taifa Bwana Vincent Minja amesema kuanzia mwaka 2026 wamejipanga kuboresha maonesho hayo yakijumuisha wadau wengi zaidi kutoka nchi zote wanachama ili kuyapa hadhi ya siku za nyuma.

Naye, Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mwanza Ndugu Gabriel Chacha amesema maonesho hayo yanaongeza mzunguko wa kifedha ndani ya nchi na kusaidia kubadilishana teknolojia kwa wafanyabiashara kutoka nchi wanachama.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA MWANZA KUCHANGAMKIA DIRISHA LA UWEZESHAJI

    September 03, 2025
  • RC MTANDA AWAASA TCCIA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZINAZOHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI

    September 02, 2025
  • WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO MWANZA WAHIMIZWA KUIMARISHA NIDHAMU ILI KUKUA KIUENDELEVU

    September 02, 2025
  • MAMLAKA ZA USIMAMIZI HUDUMA ZA MAJI NI NYENZO YA HUDUMA BORA- RAS BALANDYA

    September 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.