• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA: BENKI ZISIJENGE MAFANIKIO BILA KUWAJALI WAFANYAKAZI

Posted on: January 29th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Januari 29, 2025 amefungua rasmi Mkutano wa Mwaka wa Mameneja wa Makao Makuu na Kanda wa Benki ya NMB, uliofanyika katika Ukumbi wa Malaika jijini Mwanza, na kusisitiza kuwa mafanikio ya taasisi za kifedha yanapaswa kuanza na ustawi wa wafanyakazi wake.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Mhe. Mtanda amesema ili benki iweze kufikia malengo yake makubwa ya kibiashara na kijamii ni lazima ijenge mahusiano imara kati ya menejimenti na watumishi wa ngazi zote.

Aidha, ameipongeza Benki ya NMB kwa kuendelea kutekeleza wajibu wake kwa jamii (CSR), akibainisha kuwa zaidi ya shilingi milioni 300 zilitolewa kusaidia jamii, ambapo zaidi ya shilingi milioni 60 zilitumika kuwasaidia wagonjwa wa saratani katika Hospitali ya Kanda Bugando.

Katika hatua nyingine, Mhe. Mtanda amezitaka taasisi za kifedha kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo mkoani Mwanza, akieleza kuwa mkoa huo unachangia asilimia 7.2 ya Pato la Taifa, ukiwa wa pili kitaifa baada ya Mkoa wa Dar es Salaam.

Ameeleza kuwa utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo upanuzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwanza, ujenzi wa meli ya kisasa MV New Mwanza yenye uwezo wa kubeba abiria zaidi ya 1,200, pamoja na uendelezaji wa reli ya SGR, utaifanya Mwanza kufikika kwa njia za anga, maji na reli na hivyo kuchochea ukuaji wa uchumi wa Kanda ya Ziwa.

Pia amesema Serikali imejenga Soko Kuu la Kisasa la Mjini Kati ili kuimarisha biashara za ndani na kupunguza utegemezi wa masoko ya nje ya mkoa, hususan Kariakoo jijini Dar es Salaam.

Amehakikishia Benki ya NMB kuwa Serikali itaendelea kuiunga mkono, huku akiwahamasisha wananchi kutumia huduma za benki hiyo kutokana na mtandao wake mpana na uaminifu wake kwa jamii.

Kwa upande wake, Afisa Mkuu wa Wateja Binafsi wa Benki ya NMB, Bw. Philbert Mponzi amesema benki hiyo imekuwa ikiandaa mkutano huo kila mwaka kwa lengo la kufanya tathmini ya utendaji wa mwaka uliopita na kuweka mikakati ya utekelezaji kwa mwaka unaoendelea.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: BENKI ZISIJENGE MAFANIKIO BILA KUWAJALI WAFANYAKAZI

    January 29, 2026
  • HALMASHAURI ZAJENGEWA UWEZO UTEKELEZAJI WA DAFTARI LA MAKAZI NA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    January 28, 2026
  • TRA MWANZA YATOA MAFUNZO YA MFUMO JUMUISHI WA KODI ZA NDANI KWA WAFANYABIASHARA

    January 28, 2026
  • RAS BALANDYA APOKEA UGENI WA WIZARA YA ULINZI NA JKT MWANZA

    January 28, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.