• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza awaondoa shaka Wakazi wa Milimani Mkoani humo

Posted on: June 16th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe Mhandisi Robert Gabriel amewahakikishia wananchi wa Makaazi ya Milimani Mkoani humo kuwa wapo salama kwenye makazi yao na hakuna mtu anayeweza kuwaondoa kwenye maeneo hayo kinyume cha sheria.


Amebainisha hayo leo Juni 15, 2022 wakati akizungumza na wakaazi wa Kata ya Igogo na Pamba alipofika kusikiliza kero za wananchi hao na kukagua maendeleo ya mradi wa kuondoa maji taka kutoka kwenye makazi hayo.


"Maeneo yapo salama, mtu aliyeko juu mlimani anafanana na aliye chini wote ni sawa kwa mujibu wa sheria na ukiwa na leseni ya makazi au hati yako akija mtu analitaka eneo lako basi akuachie mahela na hakuna mtu wakukupokonya, kukufukuza wala kukudhulumu," amesema.


"Mhe Rais amefanya mambo makubwa sana kama mnavyoona huko juu kuna matenki yanaondoa maji taka na kuyaleta kwenye mfumo mkubwa huku chini na kila mtu mwenye eneo huko juu anapimiwa ardhi na kupewa leseni ya makazi ili kumhakikishia usalama wa eneo lake." Mkuu wa Mkoa amesisitiza..


"Ndugu zangu serikali imewekeza zaidi ya Bilioni 2.6 kwenye mradi wa miundombinu ya Maji Taka na unahusisha pia njia za kupanda na kushuka wananchi ambazo nimewaomba wauboreshe kwa kuweka kingo kwenye njia hizo ili wakaazi wapate kuwa salama zaidi." Mkuu wa Mkoa amesisitiza.


"Kwa upande wa kata ya Igogo na zingine tano tuna mradi wa kutambua vipande vya ardhi na kuyatambua rasmi ikiwa ni kuboresha maeneo ya vilima kwahiyo wananchi elfu 12 tumewatambua na tunawapatia leseni za makazi na wizara ya ardhi imewezesha na taarifa zinatumika kwenye mfumo wa anuani za makazi na zitatumiwa kwenye Sensa ya Watu na Makazi. Kamishna wa Ardhi Mkoa, Elia Kamihanda.


Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Mwanza, Mhandisi Martha Chuwa amesema kwa kushirikiana na serikali wanatekeleza mradi wa Maji Taka na safi na kaya zipatazo 393 kwa upande wa Igogo na maeneo mengine ambapo kwa ujumla Mradi huo umegharimu bilioni 2.6 na Umeshaanza kutekelezwa.

"Namshukuru sana Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuboreshea makazi ya wakaazi wa milimani na tumeona pale mradi wenye zaidi ya Bilioni mbili, nawahakikisha wananchi wangu hakuna atakayehamishwa." Mhe Diwani wa Kata ya Igogo Mhe Ramadhan Mahila.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.