• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali yatenga Shs Bilioni 40 Kwa ajili ya Wataalamu wa Utafiti wa mazao ikiwemo Pamba

Posted on: December 7th, 2022


Serikali katika kuhakikisha inaboresha zao la Pamba na kumuwekea mazingira rafiki Mkulima imeongeza bajeti ya Utafiti kwa Wataalamu wa kilimo kutoka Shs Bilioni 11.7 hadi kufikia bilioni 40 na bajeti ya Mbegu ikitengewa Shs Bilioni 43.

Akizungumza leo wakati wa ugawaji zana za kilimo na usafiri zenye lengo la uboreshaji wa zao la Pamba kwenye   Kituo cha Utafiti wa kilimo TARI kilichopo Wilayani Misungwi,Naibu Waziri wa Kilimo Mhe.Anthony Mavunde amesema bajeti hiyo ya utafiti imelenga pia kuboresha Maabara zote za udongo ili kumuhakikishia Mkulima uhakika wa kilimo chake na kupata mazao bora.

Amesema Serikali hii chini ya uongozi wake Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuleta mageuzi ya kweli kwenye Sekta hiyo ikitenga bajeti ya Shs Bilioni 361 ambazo zimelenga kuleta mageuzi chanya sehemu mbalimbali ukiwemo mkakati kamambe wa kuwapa ajira vijana.

"Tumeanza mradi huo kwa Vijana kuwawekea mazingira mwafaka ya kilimo kwa kuanza na Mikoa 2 ya Dodoma sehemu za Chamwino na Mbeya huko Chunya na kutenga jumla ya hekari 69000 lengo likiwa kuwafikia Vijana milioni 3  kabla ya mwaka 2030 wawe na ajira kupitia Sekta hiyo" Mhe.Mavunde

Amewakumbusha Wataalamu wa kilimo kwenye Kituo cha Utafiti Ukiriguru kuongeza ubunifu zaidi ili Mkulima azidi kupata tija kwenye mazao yake hasa Pamba ambayo ndiyo zao lenye nguvu kwenye soko la Dunia.


Ameongeza kuwa Maafisa Ugani katika kuwawekea mazingira bora ya kutoa elimu kwa mkulima wameongezewa bajeti yao kutoka Shs milioni 600 na sasa ni Shs Bilioni 15 huku wakisambaziwa jumla ya Pikipiki 7,604 zitakazo rahisisha mazingira ya kazi zao.


Akitoa taarifa za Mkoa wa Mwanza kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa huo Bw. Balandya Elikana,Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Emil Kasagara amesema Mkoa wa Mwanza msimu wa kilimo 2022/2023 unatarajia kulima zaidi ya hekta 67000 za Pamba zenye makisio ya mavuno ya Tani 56,000.


Naibu Waziri Mavunde amegawa zana za kilimo zikiwa ni baadhi kutoka kwenye mradi wa BEYOND COTTON unaofadhiliwa na Serikali ya Brazil zikiwemo mashine za kuandaa shamba 3,zana za kupandia 600, na zana za kupalilia 3 pamoja na Pikipiki 3kwa ajili ya Maafisa Ugani.


Serikali ya Tanzania Julai mwaka huu hadi Disemba 2023 imeingia rasmi mkataba na Nchi ya Brazil wa kuendeleza zao la Pamba pamoja na chakula na lishe,Taifa hilo kutoka Amerika ya Kusini likitoa Dola za Kimarekani 629,000 kugharamia mradi huo ujulikanao kama BEYOND COTTON.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.