• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Upanuzi Barabara Kukamilika Mei

Posted on: March 20th, 2018


Utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa barabara ya Makongoro hadi uwanja wa ndege unatarajia kukamilika mei 2 mwaka huu.

Mkataba wa ujenzi wa barabara hiyo uliosainiwa April 18 mwaka 2017 na M/s Nyanza Road Work Ltd ambapo gharama za mradi ni shilingi 9,542,701,531.96 unaosimamiwa na kitengo cha ushauri wa kihandisi cha wakala wa barabara TECU.

Akizungumza kwenye kikao cha pili cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Mwanza kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Meneja wa TANROADS Mkoa wa Mwanza Mhandisi Marwa Rubirya kilichofanyika jana mkoani hapa alisema, hadi sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia asilimia 74 ambapo ujenzi wa barabara hiyo kuanzia Mwaloni-Furahisha na Pasiansi hadi uwanja wa ndege upo katika hatua mbalimbali.

Mhandisi Rubirya alisema, uwekaji wa tabaka la lami ngumu imefikia urefu wa km 2.2, lami ya awali urefu wa km 2,9, tabaka la mawe yaliyosagwa urefu wa km 2.9,tabaka la msingi wa barabara km 3.1 na ujenzi wa daraja la Ilemela umekamilika kwa asilimia 90, hivyo utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kukamilika mei 2 mwaka huu.

Hata hivyo alisema, usanifu wa kina wa upanuzi wa daraja la Mabatini lililopo barabara ya Mwanza- Musoma utakamilika mwezi aprili mwaka huu na kazi inaendelea inayofanywa na Mkandarasi Mshauri M/s Advance Engineering Solution kwa gharama ya milioni 242,574.

Hatua hii ni kutokana na kuepo tatizo la mafuriko kwa muda mrefu kwenye daraja hilo pindi mvua zinaponyesha na kusababisha maji kupita juu ya barabara kwa kuwa na midomo midogo ya kupitishia maji.

Aidha, ofisi ya Meneja mkoa kwa kushirikiana na wahandisi washauri wataendelea kusimamia utekelezaji wa miradi yote ili ikamilike kwa wakati kama ilivyopangwa hivyo kwa kuiwezesha ofisi yao kutekeleza majukumu ya kujenga na kusimamia matengenezo ya barabara kama ilivyoidhinishwa katika bajeti ya wizara yao wanashauri fedha zitolewe kwa wakati.

Kwa upande wake Mratibu wa Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mkoa wa Mwanza Francisco Magoti alisema, dhima yao ni kupanga,usanifu,ujenzi, ukarabati na matengenezo ya mtandao wa barabara za vijijini na mijini kwa kuzingatia ufanisi wa gharama kwa ajili ya maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi nchini.

Alisema, TARURA ina mtandao wa barabara wenye urefu wa km 4891.56 kwa Halmashauri zote za mkoa huo,ambapo barabara ya lami km120.41,barabara ya mawe km 8.537, barabara ya zege km 2.51, barabara za changarawe km 1525,673 na barabara ya udongo km 3235,22.

Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela John Wanga aliomba kipande kitakacho baki cha barabara ya Buswelu hadi Igoma nacho kijengwe kwa kiwango cha lami, ili kuleta taswira nzuri na wananchi kufanya shughuli za uchumi kwa urahisi baada ya kukamilika kwa mradi wa barabara ya Buswelu kupitia Kiseke mpaka Sabasaba ambao unakaribia kuanza mei, huku Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mary Tesha aliwaomba TARURA kuendelea kushirikiana na wakuu wa wilaya na wabunge katika kutekeleza majukumu yao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.