• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Viwanja 50 vya ndege havina hati miliki

Posted on: July 12th, 2018


Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) imesema viwanja vingi vya ndege vimeshindwa kupata hati miliki kutokana na wananchi kuvamia maeneo hayo na kusababisha migogoro ambayo ipo kwenye vyombo vya uamuzi.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mtendaji Mkuu wa TAA, Richard Mayongela wakati akimwelezea Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Isack Kamwelwe wakati wa majumuisho ya Waziri mkoani Mwanza ambapo alisema kati ya viwanja vyote 58, vilivyo na hati ni 8.

Alisema kutokana na hali hiyo TAA imeanza kushughulikia migogoro hiyo kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambapo hadi sasa viwanja vingine vinne vipo katika hatua ya mwisho kupewa hati mmiliki na kufikisha idadi ya 12 kati ya 58.

Mayongela alisema mkakati wao ni kuhakikisha viwanja vyote nchini vinakuwa na hati miliki na ikiwezekana kuwekewa uzio ili kuepusha tena migogoro ya uvamizi.

“Nitumie fursa hii kuwasilisha kwako Mhe.Waziri changamoto zinazotukabili TAA, kwanza tumezoea kuitwa mamlaka lakini hatujapata nguvu hiyo bali kisheria tunatambulika kama wakala, sasa kutokana na hali hiyo tunashindwa kuwa na mamlaka kamili ya maamuzi, ikiwa tutapata mamlaka hayo tutaongeza utendaji Zaidi,”alisema Mayongela.

Aidha aliongeza kuwa,Mhe Waziri akiwa unapitia nakala ofisini kwake akifika kwenye kipengele hicho wanamuomba  amalizie kipengele kadhaa ili wawe na mamlaka kamili, jambo lingine ni maslahi kwa wafanyakazi ni madogo mno kwani muda mrefu hayajaboreshwa jambo ambalo linasababisha hata hali ya utendaji kwa watumishi kupungua lakini wanamshukuru Rais Dk. John Magufuli ameonyesha dhamira ya dhati katika kuboresha miundombinu ya viwanja vya ndege.

“Lipo jambo la kuboresha baadhi ya viwanja vyetu ili kuwa na vya kimataifa kwani hata ndege kubwa ya dreamline iliyokuja hivi karibuni inatua katika viwnaja vichache kama Dar es Salaam, Kilimanjaro na Mwanza, hivyo inatubidi kuendelea kuboresha na kuwa na hadhi ya kimataifa, pale Dodoma ambapo ndio makao makuu, tunatarajia kufanya maboresho ya uwanja wa Msalato ili kuwa wa kimataifa,”alisema Kamwelwe.

Mayongela alimuomba Waziri Kamwele kusaidia kukamilika mradi wa ujenzi wa uwanja wa Songwe ambao umechukua muda mrefu ili huduma ziweze kuendelea huku akitoa wito kwa Watanzania wote kuitunza miundombinu inayojengwa kwani fedha zinazotumika ni kodi ya watanzania.

Hata hivyo aliainisha viwanja vingine vinavyofanyiwa ukarabati ni uwanja wa Kigoma, Musoma, Bukoba, Shinyanga huku akisisitiza sekta ya ujenzi na uchukuzi inaendelea kuimarika kwa kasi.

Mayongela TAA inakabiliwa na changamoto ya gari la zimamoto kitendo kinachosababisha baadhi ya viwanja kutokuwa na huduma ya ndege ambapo aliongeza kwamba mpaka sasa wana gari 10 mpya ambazo zilinunuliwa katika bajeti ya 2016/2017, 2017/2018.

Pia alisema TAA imekusudia kujenga kiwanja cha ndege katika Mkoa wa Simiyu ambacho kitakuwa karibu na Hifadhi ya Taifa ya Mbunga ya Serengeti kitakachosaidia watalii wa ndani na nje kufika hapo.

Naye Waziri Kamwelwe alitoa wiki moja uwanja ndege  wa Mwanza kufanyiwa marekebisho madogo madogo kabla ya Julai 29, mwaka huu ili ndege kubwa ya dreanline iweze kutua salama.Hata hivyo alisisitiza kuendelea na uboreshaji wa jengo la abiria, zimamoto na kifaa cha hali ya hewa.

Katika hatua nyingine, Kamwelwe alisema Julai 29, mwaka huu atakuwa Mwanza kwa ajili ya kuingia mkataba wa ujenzi wa ukuta kuzungushia uwanja wa ndege pamoja na uzinduzi wa Kivuko cha MV Mwanza ambacho kitafanya safari zake kati ya Busisi-Kigongo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.