• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO MWANZA WAHIMIZWA KUIMARISHA NIDHAMU ILI KUKUA KIUENDELEVU

Posted on: September 2nd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wafanyabiashara ndogondogo mkoani humo kuwa na nidhamu ya shughuli zao ili kuendeleza  mitaji na kupata faida zenye tija.

Ametoa wito huo leo Septemba 02, 2025 wakati akihutubia katika kongamano la wafanyabiashara ndogo ndogo wa Mkoa huo lililowakutanisha makundi mbalimbali wakiewemo Machinga, Maafisa Usafirishaji (Bodaboda & Bajaji), Wasusi, Washonaji, Mama Lishe, Baba Lishe na waendesha Guta.

Mhe. Mtanda amesema biashara inahitaji kujielimisha hususani masuala ya mitandao ili kujua ni taasisi gani inatoa hifadhi ya jamii na waweze kujiunga pamoja na kujihakikishia ulinzi wa mitaji kwa kujisajili kwenye bima kama za moto na ajali.

Aidha, amewapongeza wajumbe wa kongamano hilo kwa kupata elimu ya masuala mbalimbali hususani kuzifahamu taasisi za kifedha zinazokopesha mitaji na akatoa wito kuzingatia elimu iliyotolewa na Mamlaka ya Usimamizi wa Bima nchini (TIRA) ili kulinda biashara zao.

“Mtembea bure sio sawa na mkaa bure, mmejifunza mengi na nawapongeza waandaaji wa kongamano hili kwa kugusa kila rika na kundi kuhakikisha wanawajengea uwezo katika masuala mbalimbali, nendeni mkayafanyie kazi na kuwafikishia wengine elimu mliyopata.” RC Mtanda.

Vilevile, ametumia wasaa huo kuwaalika kushiriki Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025 kwa kuanza kushiriki kwenye kampeni na uchaguzi wenyewe kwa amani na utulivu.

Akisoma risala ya wafanyabiashara ndogondogo Ndugu Aziz Jabir ametumia jukwaa hilo kutoa shukrani kwa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwajengea ofisi katika Mikoa yote na kuwaletea vitambulisho vinavyowafanya watambulike na kupewa mikopo na taasisi za kifedha kote nchini.

Aidha, ameipongeza serikali kwa kuchochea shughuli zao kwa uboreshaji wa miundombinu ya barabara, Maji, Bandari, Reli na Vivuko nchini na akabainisha changamoto ya usajiri unaolegalega kwani ni wafanyabiashara elfu 2 pekee kati ya zaidi ya elfu 6 waliopo Mwanza ndio wamesajiriwa na kukwamisha ukopaji wa fedha za mitaji.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA MWANZA KUCHANGAMKIA DIRISHA LA UWEZESHAJI

    September 03, 2025
  • RC MTANDA AWAASA TCCIA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZINAZOHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI

    September 02, 2025
  • WAFANYABIASHARA NDOGO NDOGO MWANZA WAHIMIZWA KUIMARISHA NIDHAMU ILI KUKUA KIUENDELEVU

    September 02, 2025
  • MAMLAKA ZA USIMAMIZI HUDUMA ZA MAJI NI NYENZO YA HUDUMA BORA- RAS BALANDYA

    September 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.