• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Wananchi wanao ishi jirani na mradi wa Ihelele Wilayani Misungwi watakiwa kutunza mazingira

Posted on: March 10th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima amewataka wananchi wanaozunguka kulinda chanzo cha Maji Ziwa Victoria Ihelele  kwenye Kijiji cha Nyangomang'ho kata ya Ilujamate kutunza chanzo hicho kinachohudimia wananchi takribani 1,250,000 (2021) kwenye Mikoa mitano.

Akikagua Mradi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama-Shinyanga (KASHWASA) unaozalisha takribani mita za Ujazo 63,000 kwa siku, leo Machi 02, 2023 Mhe. Malima amesema jamii ina wajibu wa kuutunza mradi huo kwa dhati na kujiepusha na shughuli za kiuchumi zinazochafua Maji na kuharibu mazingira.


"Huu mradi ni wa kitaifa, watanzania wengi wanapata maji kutoka hapa Ihelele, siku za nyuma nilipata kusikia kuwa Maji yanayotumika Tabora yanatoka kwenye Chanzo cha Ihelele na leo nimefurahi kufika hapa na kuuona mradi huu kwa macho yangu mwenyewe." Malima.

Mkurugenzi wa Bonde la Ziwa Victoria Mhandisi Renatus Shinhu amesema taasisi hiyo imepanda Zaidi ya Miche ya Miti elfu 8 na kwamba pamoja na afua zingine wametumia Zaidi ya Milioni 250 kuhifadhi mazingira ya bonde hilo na imesadia kuongeza ubora wa Maji na kurejesha na uoto wa asili ambao ulianza kutoweka.

"Chanzo hicho kinakabiliwa na uharibifu wa Mazingira ukiwemo ufugaji wa kilimo ndani ya hifadhi, ukataji wa miti kwa ajili ya kuni, uchomaji wamkaa na matofali na uvuvi wa samaki usio endelevu na kwamba hayo yanasababisha uchafuzi wa chanzo na kupelekea kuongezeka kwa gharama za kutibu Maji." Mhandisi Shinhu.

Aidha, Mkurugenzi huyo amebainisha kuwa ziwa Victoria lina ukubwa wa Kilomita za Mraba 68,800 na kwa upande wa Tanzania ni 35,700 na kwamba ziwa hilo lima Maji kiasi chan Mita za Ujazo Bilioni 2,700 na ka upande wa Tanzania ni Bilioni 1,400.

Naye, Mkurugenzi wa Mamlaka ya majisafi na Usafi wa Mazingira Kahama-Shinyanga (KASHWASA) Mhandisi Patrick Nzamba amefafanua kuwa chanzo hicho kina uwezo wa kuzalisha Lita Milioni 80 hadi 120 kwa siku na kwamba kwa sasa wanazalisha Lita Milioni 63 na kwamba gharama kubwa za uzalishaji na wateja kutolipa kwa wakati Ankara zao zinaathiri uendeshaji wa mradi.

Chanzo cha Maji ziwa Victoria Ihelele kinatumiwa na Mamlaka ya KASHWASA kusambaza Maji katika Mamlaka zilizopo katika Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Geita, Tabora, Singida na Simiyu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.