• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAZIRI MKUU KUZINDUA MELI YA KISASA MWANZA KESHO

Posted on: January 22nd, 2026

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba (MB) anatarajiwa kuzindua Meli ya kisasa ya MV. New Mwanza katika Bandari ya Mwanza Kusini kesho ijumaa tarehe 23 Januari, 2026.

Hayo yamebainishwa na Mhe. Prof. Makame Mbarawa (MB), Waziri wa Uchukuzi leo tarehe 22 Januari, 2026 wakati akizungumza na Waandishi wa Habari katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Prof. Mbarawa amesema Meli ya MV Mwanza imejengwa na Mkandarasi Gas Entec Ship- Building kutoka Korea kwa kushirikiana na Kampuni ya Meli nchini (TASHICO) kwa gharama ya Tshs. Bilioni 120.56.

Amefafanua kuwa Ujenzi wa Meli hiyo umezingatia teknolojia ya juu na kwamba mpaka sasa meli hiyo imefanyiwa safari sita za majaribio (Mwanza - Bukoba) kuanzia mwezi Machi 2025 ambapo majaribio hayo yameonesha ufanisi mkubwa na TASAC imeridhika na ubora na kuruhusu kuanza kwa safari.

Aidha, ameongeza kuwa Meli hiyo ya ghorofa 4 ndiyo kubwa zaidi ya zote ndani ya ukanda wa maziwa makuu na ina uwezo wa kubeba abiria 1200, tani 400 za mizigo, magari madogo 20 pamoja na makubwa 3 kwa wakati mmoja.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametumia wasaa huo kuwakaribisha wananchi wa Mkoa huo pamoja na mikoa ya jirani kumlaki na kushiriki kwenye ziara hiyo ya kitaifa ya Mhe. Waziri Mkuu kuanzia saa 2 asubuhi.

Mhe. Mtanda amebainisha kabla ya Mhe. Waziri Mkuu kuzindua mradi huo ataanza na Ukaguzi wa mradi wa Ujenzi wa kituo cha kuratibu ufuatiliaji na uokozi katika ukanda wa ziwa Victoria katika eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwanza wilayani Ilemela.

Ameongeza kuwa baada ya hapo Mhe. Waziri Mkuu ataweka pia jiwe la Msingi katika Mradi wa Ujenzi wa Matenki, Vituo vya Kusukuma Maji na Mabomba Makuu katika Mtaa wa Sahwa kata ya Lwahnima Jijini Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MTAKUWAA MWANZA YAWEZESHA KUPUNGUZA WATOTO WA MTAANI KWA 50%

    January 26, 2026
  • RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

    January 26, 2026
  • NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.