• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

ZAIDI YA BILIONI 2 KUNUFAISHA WANANCHI UJENZI WA MINARA YA MAWASILIANO MWANZA

Posted on: July 18th, 2024

ZAIDI YA BILIONI 2 KUNUFAISHA WANANCHI UJENZI WA MINARA YA MAWASILIANO MWANZA


Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Nape Nnauye (MB) amesema Serikali inatekeleza mradi wa ujenzi wa minara 758 unaogharimu zaidi ya Bilioni 200 utakaonufaisha wananchi Milioni 23.6 kupata huduma bora za mawasiliano ya intaneti, data na simu.

Mhe. Nape amebainisha hayo leo Julai 18, 2024 Wilayani Sengerema alipokua ziarani kukagua mnara wa mawasiliano katika Kisiwa cha Lyakanyasi huku akibainisha kuwa wilaya hiyo itanufaika kwa kujengewa minara 2 kati ya 17 inayojengwa Mwanza.

"Minara hii inajengwa na makampuni ya simu tena inagharimu fedha nyingi sana zaidi ya Milioni 350 kwa mnara mmoja tena kwenye maeneo ambayo hayana mvuto sana kibiashara na kwakweli makampuni mengine yasingeweza kwenda kuwekeza hivyo ni lazima ilindwe." Mhe. Nnauye.

Vilevile, amewasihi viongozi wa wilaya kusimamia upatikanaji wa maeneo ya kujenga minara hiyo itakayosaidia kukuza uchumi vijijini na akatoa wito kwa taasisi zinazotoa huduma za umeme na barabara  kufikisha miundombinu hiyo kwa kipaumbele ili kurahisisha utoaji wa huduma bora pamoja usalama.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutenga zaidi ya Tshs. Bilioni 2.4 kwa ajili ya kujenga minara 17 katika kata 16, vijiji 52 na inatarajiwa kunufaisha zaidi ya wananchi 296, 410 wa wilaya 5 za Magu, Ilemela, Sengerema, Misungwi na Ukerewe.

Akiwasilisha taarifa ya Mamlaka ya Mawasiliano nchini (TCRA) John Dafa amesema hali ya mawasiliano nchini ni ya kuridhisha kwa zaidi ya asilimia 85 (2G, 3G, 4G) na kwa Mwanza huduma zimefika kwa wananchi kwa wastani wa zaidi ya asilimia 95.

Akizungumzia usajili wa laini za simu amesema Mwanza kuna ongezeko la zaidi ya asilimia 42 kutoka mwaka 2022 kwani wananchi 4,803,249 (Machi 2024) wamesajiliwa kutumia laini za simu na kwamba kuna zaidi ya vituo vya redio 26 mkoani humo kwa sasa.

Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Bi. Justina Mashiba amesema hakuna mtanzania atakaa bila huduma za mawasiliano na kwamba siku za nyuma minara 50 ilijengwa kupitia ruzuku ya awali UCSAF kwa zaidi ya Bilioni 6.6 huku wananchi 885, 420 wakinufaika mkoani Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.