• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

CP. Mtweve atangaza Matokeo ya Mtihani Elimu ya Msingi

Posted on: December 12th, 2017

Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza CP.Clodwig Mtweve ametoa Taarifa ya Matokeo ya Mtihani wa kumaliza Elimu ya Msingi (PSLE 2017) Katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

CP. Mtweve amesema kuwa Mkoa wa Mwanza umepata ufaulu wa wa asilimia 77.3 ambapo kati ya watahiniwa wote 70368 waliofanya Mtihani huo ni watahiniwa 54367 ndio waliopata alama za ufaulu yaani kati ya alama 100 mpaka alama 250.Ameongeza kuwa kati ya watahiniwa waliofaulu wavulana ni 27971 na wasichana ni 26396 hali iliyopelekea Halmashauri zote 8 kupata za Mkoa wa Mwanza kupata ufaulu zaidi ya asilimia 50.

Aidha ufaulu katika Halmashauri zilizopo Mkoa wa Mwanza ni kama ifuatavyo ambapo Halmashauri ya Jiji la Mwanza 88.7% ,Ilemela 87.5%,Buchosa 85.8%,Sengerema 82.3%,Misungwi 79.4%,Kwimba 73.7%,Magu 71.6% na Ukerewe 50.7%.

Ufaulu wa Shule 10 Bora Kimkoa kundi la Watainiwa zaidi arobaini (40+) Shule ya Alliance imekuwa ya kwanza Kiwilaya na Mkoa ya Kwanza wakati Kitaifa imekuwa ya tatu, Mugini imeshika nafasi ya kwanza kiwilaya wakati Kimkoa imekuwa ya pili na Kitaifa imekuwa ya 15.Kazungu imekuwa uya 1 kiwilaya ya 3 kimkoa na imeshika nafasi ya 25 Kitaifa.Shule ya Msingi Nyamuge imekuwa ya 1 Kiwilaya ya 4 Kimkoa na imeshika nafasi ya 30 Kitaifa.

Shule ya Msingi Tulele imeshika nafasi ya 2 Kiwilaya ya 5 Kimkoa na Kitaifa imeshika nafasi ya 31. Lake View imekuwa ya 3 Kiwilaya ya 6 na Kitaifa ni ya 45. Kimiza imekuwa ya 1 Kiwilaya ya 7 katika Mkoa na 58 Kitaifa. Buswelu imekuwa ya 2 Kiwilaya ya 8 Kimkoa na Kitaifa imeshika nafasi ya 62. New Alliance imekuwa ya 2 Kiwilaya ya 9 Kimkoa na imeshika nafasi ya 75 Kitaifa wakati Shule ya Msingi Eden ni ya 4 Kiwilaya ya 10 Kimkoa na Kitaifa ni ya 77.

Shule za Msingi 10 dhaifu kwa kundi la watahiniwa zaidi ya 40 zimetajwa kuwa ni Muriti,Kaseni,Kazilankanda,Negoma,Mugu,Chamatuli,Mahande na Busagami zote za Ukerewe na Kidija na Mhalo zote za Kwimba.

Ufaulu wa Shule10 bora Kimkoa kundi la Watainiwa chini ya arobaini (40-)

Shule ya Msingi Musabe ya Jiji la Mwanza imeshika nafasi ya 1 kiwilaya ya 1 Kimkoa na Kitaifa imeshika nafasi ya 4.Peaceland ya Ukerewe imeshika nafasi ya 1 Kiwilaya ya 2 Kimkoa na ya 26 Kitaifa,Lowjoma ya Manispaa ya Ilemela imeshika nafasi ya 1 Kiwilaya,3 Kimkoa na Kitaifa nafasi ya 31,Lake Victoria E.M ya Buchosa imeshika nafasi ya 2 Kiwilaya ya 4 Kimkoa na nafasi ya 34 Kitaifa, Methodist ya Magu imeshika nafasi ya 1 Kiwilaya,5 Kimkoa, na 39 Kitaifa.

Central Buhongwa ya Jiji la Mwanza nafasi ya 2 Kiwilaya,6 Kimkoa na 62 Kitaifa,Winners ya Jiji la Mwanza imeshika nafasi ya 3 Kiwilaya,7 Kimkoa na 69 Kitaifa,Exodus ya Misungwi nafasi ya 1 Kiwilaya,8 Kimkoa na 71 Kitaifa,Kisiwani ya Jiji la Mwanza nafasi ya 4 kiwilaya,9 Kimkoa,74 Kitaifa na Mahawa Independent ya Jiji la Mwanza imeshika nafasi ya 5 Kiwilaya,10 Kimkoa na 75 Kitaifa.

Shule za Msingi 10 dhaifu Kimkoa kundi la watahiniwa chini ya 40 zimetajwa kuwa ni Bugatu ya Magu,Nyabuhere ya Misungwi,Mwabudi ya Kwimba,Isesa ya Ilemela,Ng’wang’hanga ya Kwimba,Kilongo ya Ukerewe,Ndagwasa ya Kwima na Itegamatu ya Kwimba.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.