• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

WAHITIMU WA SAYANSI NA TEKNOLOJIA WANATEGEMEWA SANA NA SERIKALI- MHE. WANU

Posted on: December 15th, 2025

Naibu Waziri wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Wanu Ameir (Mb) amesema wahitimu wa masomo ya Sayansi na Teknolojia wanahitajika kwa wingi zaidi nchini kwani Uchumi unategemea zaidi ujuzi wenye ubunifu, sayansi na teknolojia.

Ameyasema hayo leo Desemba 15, 2025 katika mahafali ya 19 duru ya pili ya chuo cha Taasisi ya Teknolojia Dar es salaam (DIT) kampasi ya Mwanza wakati akitunuku vyeti kwa wahitimu wa Astashahada na Stashada katika fani mbalimbali kwa niaba ya Waziri wa Wizara husika.

Aidha, Mhe. Wanu ameeleza kuwa katika kuongeza fursa kwa vijana serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imeleta mradi wa DISTIC wenye thamani ya Billioni 37 chuoni hapo ili utakaofadhili mambo kadhaa ikiwemo ujenzi wa kiwanda cha kufundisha na kuchakata bidhaa.

Vilevile, amezitaja juhudi zingine za kuboresha ufundi stadi kuwa ni pamoja na uwepo wa Bilioni 15.27 zilizopatikana kupitia mradi wa TERMS II zilizotolewa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia kwa vyuo vingine vya ufundi nchini.

Akiupongeza uongozi wa chuo hicho hasa kwa kushirikiana na mataifa kama Uingereza, Ureno na Ethiopia Mhe. Wanu ameeleza kuwa serikali imeendelea kuwajengea uwezo watumishi wa taasisi za elimu ya ufundi stadi nchini kwa kutoa wakufunzi 912 wa mitaala inayoendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Naye Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Said Mtanda amewasihi kupunguza kutoa mafunzo ya baadhi ya kada ili kujikita katika taaluma ambayo wahitimu watakapomaliza waweze kujiajiri na sio kujenga idadi kubwa ya wenye vyeti bila maarifa, ujuzi na ubunifu.

Halikadhalika, amewapongeza wahitimu na kuwataka na kuwasihi kujiunga kwenye vikundi na kuchukua mikopo serikalini isiyo na riba na kujenga vizimba vya kufugia samaki ili kumudu maisha kwani wamepata stadi za nadharia kwenye eneo hilo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AFANYA KIKAO NA NAIBU WAZIRI TAMISEMI (AFYA)

    December 16, 2025
  • WAHITIMU WA SAYANSI NA TEKNOLOJIA WANATEGEMEWA SANA NA SERIKALI- MHE. WANU

    December 15, 2025
  • WAKUU WA VITENGO MIKOA WATAKIWA KUTEKELEZA MIRADI KIZALENDO ILI KUCHOCHEA MAENDELEO

    December 12, 2025
  • WAZIRI ULEGA AWASILI MWANZA KUTEKELEZA AGIZO LA PM UKAGUZI MADARAJA

    December 11, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.