• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Elimu ya Afya yatolewa Mwanza

Posted on: May 8th, 2021

Wito umetolewa kwa watu wenye tatizo la shinikizo la damu kufanya mazoezi na kuepuka ulaji usiopangiliwa huku tahadahari ikitolewa kwa wanaojikita kutumia tiba asili ambazo hazijafanyiwa utafiti.

Wito huo umetolewa na Daktari bingwa mbobezi wa magonjwa ya figo na shinikizo la damu wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Ladislaus Rudovick,wakati hospitali hiyo ikiadhimisha siku ya Shinikizo la Damu Duniani kwa kutoa huduma za upimaji afya bure kwa magonjwa yasiyoambukiza.

Dkt.Rudovick alisema,suluhisho la kwanza kwa mtu mwenye tatizo la shinikizo la damu ni kufanya mazoezi na kuepuka ulaji usiopangiliwa.


Huku akitoa tahadhari kwa wale wanaojikita zaidi kwenye tiba asili ambazo hazijafanyiwa utafiti kwani moja ya  changamoto ni kupata madhara mengine yanayoweza kusababisha matatizo zaidi ya kiafya, ikiwemo kuharibu figo.


Akizungumzia ugonjwa wa shinikizo la damu Dkt.Rudovick, alisema ugonjwa huo umegawanyika katika sehemu kuu mbili ambapo ya msingi hubainika zaidi kwa wale wenye umri wa kati ya miaka 30 hadi 50 na chanzo chake kwa asilimia 90 hadi 95 huwa hakijulikani.

Huku ya sekondari ni chini ya umri wa miaka 30 au zaidi ya miaka 55 ambayo chanzo chake hujulikana na wakiondoa chanzo basi tatizo linakwisha jumla.

Alisema,baadhi ya  visababishi  ni pamoja na mishipa ya kwenye figo kuwa miembamba, uvimbe tumboni na matatizo ya tezi yanayopelea homoni mwilini kuongezeka pamoja na mfumo wa maisha ambao  unaweza kuwa chanzo kikubwa hasa kwa watu wenye kipato kizuri kinachopelekea ulaji usiopangiliwa pamoja na kukosa muda wa kufanya aina yoyote ya mazoezi.


“Utakuta mtu anatoka ndani kwake na kuingia kwenye gari hadi ofisini huku muda wa kazi ukiisha anaingia tena kwenye gari, anapita sehemu za burudani, anaagiza nyama, tena ile nyekundu na kileo, hasa bia, kisha anarudi nyumbani anaoga na kulala, na kesho yake hivyo hivyo,”alisema.


Kwa upande wake  Daktari Nelly Mwageni,alisema magonjwa ya ngozi  nayo pia huendana na umri wa mtu ambapo  watoto chini ya umri wa miaka 12 wao husumbuliwa zaidi na pumu ya ngozi ambayo chanzo chake mara nyingi ni kurithi kutoka katika ukoo na baadhi ya dalili ni kuwashwa macho na mafua ya mara kwa mara.


“Mara nyingi hujitokeza kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa,mwingine mvua nyingi au joto kali ni tatizo na mwingine msimu wa mazao kutoa maua ni shida,mfano ule ungaunga unaotoa maua ya mahindi ukimpata mtoto wa tatizo hilo anaathirika,” alisema.


Ambapo vijana mara nyingi hupatwa na tatizo la mba na chunusi kutokana na balehe, wazee ni ngozi kuwa kavu kutokana na upungufu wa uwezo wa mwili kuzalisha mafuta.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.