• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mongella akagua Shughuli za Maendeleo,atoa maagizo kwa watendaji

Posted on: April 29th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe  John Mongella amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya  Magu Mkoani Mwanza,kuhakikisha jengo jipya la wagonjwa wa nje(OPD)la  hospitali ya halmashauri hiyo linakamilika kabla ya Juni 30, mwaka huu.

Mhe.Mongella alitoa agizo hilo  mara baada ya kutembelea hospitali hiyo wakati wa ziara yake ya kukagua shuguli za maendeleo Wilayani Magu ikiwemo hospitali hiyo, mradi wa maji Magu mjini,REA Bugabu na Bonde la Kandawe kwa ajili ya kuangalia shughuli za kilimo cha mpunga, alisema hawawezi kuwa na kitu kimoja tu hivyo wamalizie jengo hilo ili waanzishe suala jingine.

Mhe.Mongella alisema, Mkurugenzi anapaswa kuhakikisha anakamilisha jengo hilo kabla ya kuanza kwa mwaka mpya wa fedha wa kiserikali ili liweze kutoa huduma kwa wananchi.

"Jitahidi kabla ya kuanza mwaka mpya wa fedha uwe umekamilisha jengo hili,ambapo tutamualika Waziri Mkuu au Rais akiwa anapita atuzindulie jengo letu na wananchi waanze kupata huduma kupitia katika jengo hilo," alisema Mongella.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Magu George Lutengano, alisema ofisi ya Rais TAMISEMI iliwaletea fedha milioni 200,kwa ajili ya kufanya ukarabati wa jengo la wagonjwa wa nje la zamani,lakini ni chakavu na wakafikiri siyo busara kuweka fedha hizo katika jengo hilo ambalo ata ukarabati wake usinge onekana vizuri.

Hivyo waliona fedha hizo kujenga jengo jipya kwa ajili ya wagonjwa wa nje ambapo waliwasiliana na Wizara wakawahaidi kuwa watawaongezea fedha ili kukamilisha ujenzi huo,lakini wakiwa wanasubilia fedha hizo hawawezi kukaa hivyo watakata fedha za mapato ya ndani ya halmashauri na zinazokusanywa kutoka hospitali ili kuendelea kufanya kile kinachowezekana.

"Mkuu wa Mkoa ametushauri kuwa vyovyote tutakavyo fanya tujitahidi ili jengo kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha basi liwe limeisha na kuweza kutoa huduma kwa watumishi na wananchi kwani jengo tulilonalo kwa sasa hali yake siyo nzuri,kimsingi tulivyopata milioni 200 wengine walituambia kuwa hatuwezi kujenga hili jengo kama mnavyoliona,mimi sipendi kukata tamaa tutakaa na wenzangu tutafanya linalowezekana tunaona tunatekeleza maelekezo ya Mkuu wa Mkoa ili liweze kutoa huduma kwa maslahili ya wananchi wetu ambao wanahangaika,tutapigana na tutafika tunapo fika ili watu waanze kupatiwa huduma hapa ifikapo Julai," alisema Lutengano.

Hata hivyo alisema,jengo hilo litaweza kuwahudumia wagonjwa wote wa rufaa wanaoletwa kwa ngazi  ya Wilaya kwa sababu kuna vyumba vya madaktari vya kuona wagonjwa siyo chini ya 8,chumba kidogo cha upasuaji,vyumba vya wauguzi na dawa,ni la kisasa ambalo limezingatia ramani mpya iliyotolewa na ofisi ya Rais TAMISEMI,hivyo wanaamini lutakidhi mahitaji ya wananchi wa Magu litakapo kamilika ambapo ujenzi umechukua miezi mitano na hiyo ni kutokana na uhaba wa fedha.

Nao baadhi ya wananchi wa Wilayani Magu, walisema endapo jengo hilo litakamilika litawasaidi kupunguza msongamano na kupata huduma kwa haraka,hivyo walimshukuru Mhe. Rais kwa juhudi zake za kuwasaidia wananchi na kuboresha sekta ya afya ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya na dawa.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.