• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

MWANZA BILA YA WATOTO WA MITAANI INAWEZEKANA: RC MAKALLA

Posted on: March 15th, 2024

MWANZA BILA YA WATOTO WA MITAANI INAWEZEKANA: RC MAKALLA


*Kampeni maalum ya mchukue mtoto mrejeshe kwa wazazi wake imeanza Mwanza*


*Zaidi ya watoto mia tano wamerejeshwa nyumbani*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla amesema Ofisi yake kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wapo katika kampeni maalum ijulikanayo kama 'Mchukue mtoto mrejeshe kwa wazazi wake' yenye lengo la kuwaondoa watoto mitaani na kurudi kwenye malezi bora.

Akizungumza leo kwa niaba yake na kamati ya kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi amesema kupitia kampeni hiyo kuna matarajio ya kupata matokeo chanya huku wakiwa wamefanikiwa kuwarejesha kwa wazazi wao zaidi ya watoto mia Tano.

"Mhe. Mwenyekiti wa Kamati kampeni hii tunashirikiana vizuri na wadau wa maendeleo wanaojishughulisha na watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu, kabla ya kuwarejesha huwa tunajiridhisha sababu za watoto hao kutoroka nyumbani kwao," Mhe. Makilagi

Makilagi amesema kwenye Stendi ya mabasi ya Nyegezi wameweka dawati maalum ya Ustawi na kufanikiwa kuwarejesha nyumbani watoto 223 na sasa wapo mbioni kuyaweka madawati mengine kituo cha mabasi Nyamhongolo, bandarini na eneo la Kamanga Feri.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Mwanaidi Hamis amesema Serikali inaendelea kuiboresha miundombinu yote iliyo chini ya Wizara hiyo kikiwemo chuo cha Maendeleo ya Jamii Misungwi zilizotokewa shs bilioni 2.2 kujenga bweni la wanafunzi.

"Tayari zimetolewa shilingi Milioni 350 kuanza kujenga msingi na katika ziara hii waheshimiwa wabunge wa kamati hii watapita kukagua ujenzi huo", Amesema Naibu Waziri.

Mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye ni Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Dodoma, Mhe. Fatma Tawfiq amebainisha jukumu la jamati yake ni kupita kwenye miradi yote na kujiridhisha kuona thamani ya fedha zilizolengwa zimeendana na kilichokusudiwa.

"Sisi wabunge ndiyo tunapitisha bajezi za Serikali na kutoa ushauri pia kwenye miradi iliyokusudiwa ya kuwaletea maendeleo wananchi, hivyo ziara hii ina maana kubwa," Mwenyekiti wa kamati.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SEKTA BINAFSI MWANZA

    May 10, 2025
  • SERIKALI KUNUNUA MTAMBO RASMI WA KUSAFISHA ZIWA VICTORIA

    May 10, 2025
  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.