• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Mwanza Yajipanga kutokomeza ongezeko la watoto wa mitaani

Posted on: November 15th, 2019

Mwanza Yajipanga kutokomeza ongezeko la watoto wa Mitaani


Wizara ya Afya kupitia idara kuu ya Maendeleo ya Jamii kwa kushirikiana na Mkoa wa Mwanza wameweka mikatati ya pamoja ya   kuunganisha watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani ili kurudi katika familia zao.

Akizungumzia ongezeko la watoto wa Mitaani Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.John Mongella amesema kupitia tafiti zilizofanywa na Head Count lililoendeshwa na wadau wa Railway Children Africa na Cheka sana Tanzania 2017 umetambua  jumla ya watoto 1254 walio katika mitaa yetu, 978  walitambuliwa wakati wa mchana na usiku ni watoto 276 kuwa wanalala na kufanya shughuli mbalimbali za mitaani wakati wa usiku.

"Kuna haja ya kutambua hawa watoto kwa kupitia viongozi wa vijiji, mitaa na vitongoji na  mimi naunga mkono sana Mwanza tuko tayari kama ni kuanza kulikabili, tupo tayari kushirikiana na Wizara,wadau wote na si kwa maana ya  kuwanyanyasa bali kuwajenga  wawe raia wema kwenye jamii hata kwenye Taifa.

Aidha ameyataadharisha mashirika na wadau wanaotoa misaada kwa watoto wa mitaani ambayo huwasaidia wiki nzima na kukiri kuwa  inaongeza ongezeko la watoto wa mitaani kwani wanapata mahitaji, hivyo amewaomba wadau waungane ili kuwarudisha majumbani.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee  na Watoto  Dkt. John Jingu amesema zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo la watoto kuja mitaani ambazo ni pamoja na vifo vya wazazi au walezi wa watoto,ugomvi wa wazazi na malezi potofu yasiyojali haki za watoto, ukatili pamoja na umaskini kutoka kwenye familia.

"Sheria imeeleza majukumu ya makundi mbalimbali katika kumlea mtoto ambapo kati ya makundi haya ni familia,jamii na mamlaka za Serikali za Mitaa,hivyo wafundishwe malezi sahii ya kustawisha jamii zetu,"alisema Dkt.Jingu.

"Kuweka kumbukumbu za watoto waishio katika mazingira hatarishi, pia kufanya ufuatiliaji wa watoto hao, wafanyiwe uchunguzi pia tukubaliane warudishwe majumbani kwao  kwani sheria ya mtoto ya mwaka 2009 inaruhusu," alisema  Dkt.Jingu.

Kwa upande wake Kamishna wa Ustawi wa Jamii Dkt.Naftali Ng'ondi awali akiwakaribisha wadau katika kikao amesema Wizara  yetu ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto kwa muda mrefu imekuwa na mazungumzo na Mkoa wa Mwanzajuu ya kuwa na mpango kabambe na endelevu wa kushughulikia tatizo la watoto wanaoishi katika mazingira hatarishi.

" Mpaka sasa kwa mujibu wa Taarifa ambazo tunazo una jumla ya watoto 1254 ambao wanaishi na kufanya kazi mitaani,tunafahamu kwamba takribani asilimia 90 tunawafahamu wazazi wao, hivyo tumekutana hapa kuja kujadili na kuja na mpango ambao utatuwezesha kulishughulikia tatizo hili vizuri zaidi,"alisema Dkt.Ng'ondi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.