• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MAKALLA ATANGAZA VITA NA MAMBO 10 KUKOMESHA UVUVI HARAMU MWANZA

Posted on: December 21st, 2023

RC MAKALLA ATANGAZA VITA NA MAMBO 10 KUKOMESHA UVUVI HARAMU MWANZA


*Atangaza siku 7 za kurejesha zana haramu na msako mkali utafuata*


*Awataka Maafisa uvuvi kusimamia sheria kutimiza wajibu wao*


*Awataka viongozi ngazi zote kutimiza wajibu kwa kutoa elimu ya uvuvi haramu*


*Awaagiza viongozi kulinda mazalia ya Samaki na ziwa kwa ujumla*


*Azitaka Halmashauri kuwa na bajeti ya ufuatiliaji sekta ya uvuvi*


*Ampongeza Mhe. Rais kwa kutoa bilioni 65 kuwezesha uvuvi wa kisasa 2022/23*


*Abainisha kuwa uwanja wa ndege wa Mwanza kusafirisha ninofu ya Samaki nje ya nchi*


Leo Disemba 21, 1023 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. CPA Amos Makalla ameongoza kikao kazi cha wadau wa uvuvi na ametoa siku saba za kurejesha zana haramu za uvuvi na kwamba baada ya hapo msako mkali utafanyika na kuwakamata wote wanaojihusisha na uovu huo ili wachukuliwe hatua za kisheria.

CPA Makalla amesema ifikapo Disemba 30 msako mkali wa kuwakamata wote wanaojihusisha na uvuvi haramu na watafikishwa kwenye vyombo vya sheria na kwenye kuthibiti hilo amewataka Maafisa uvuvi kuwajibika ipasavyo katika kutoa elimu dhidi ya madhara ya uvuvi haramu ili kukomesha zana na mbinu haramu kwenye ukanda wa ziwa Victoria.


"Hii sio nzuri hasa visiwani, ni lazima wataalam tuwe na Mkakati endelevu wa kuthibiti uvuvi haramu na kurejesha ziwa kwenye hali ya asili ni lazima tuwe na uvuvi endelevu kwa kutumia zana zinazokubalika kwenye kuvua na si vinginevyo ili kuokoa soko, ubora na ajira za watanzania wengi wanaoendelea kuathirika kutokana na matendo hayo." Amesema Mkuu wa Mkoa.

Aidha, amesema uwepo wa masoko ya bidhaa zisizokubalika ndio chanzo cha uvuvi haramu hivyo jeshi la polisi na mamlaka zingine zizuie suala hilo na ni lazima elimu itolewe mara kwa mara kuelezea madhara ya uvuvi haramu kwa maendeleo ya ziwa hilo linalotegemewa kwa ukuzaji uchumi.


"Mwaka 2022/23 Serikali imetoa bilioni 65 kuwezesha wavuvi kwa kuwakopesha boti 158 zenye vifaa vya uvuvi ambapo Mwanza imepata  boti 29 pamoja na mradi wa vizimba 615 kwa kufugia samaki ambapo Mwanza imepata vizimba 375" Amefafanua Mkuu wa Mkoa.


Mtafiti Mwandamizi kutoka Taasisi ya utafiti wa Uvuvi nchini (TAFIRI) Hillary Mrosso amebainisha kuwa utafiti kwa njia ya teknolojia ya uwingi unaonesha kuwa wingi wa samaki aina ya Sangara umepungua kutoka tani 621, 254 mwaka 2015 hadi tani 161, 918 mwaka 2022 huku miaka ya 2018, 2021 na 2022 ikiongoza.

"Uwingi wa dagaa umeonekana kupungua kutoka tani 859, 931 mwaka 2015 hadi 321, 392 mwaka 2017 na kwamba uwingi wa uduvi umekua ukiongezeka katika vipindi mbalimbali." Amefafanua Mtafiti Mwandamizi Mrosso.


Akitoa wasilisho la sekta ya uvuvi, Afisa uvuvi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Titus Kilo amesema uzalishaji wa mazao ya samaki kwenye viwanda mkoani Mwanza umepungua kwa asilimia 30  kwa siku kutoka tani 455 hadi 319 na hali hiyo imepelekea kupungua kwa siku  kufanya kazi hadi siku 3 kwa wiki huku wafanyakazi wakipungua kutoka 3600 hadi 1800.


"Usafirishaji wa mazao ya uvuvi nje ya nchi umepungua kutoka tani 8, 356 kwa mwaka 2021/22 hadi tani 7, 112 mwaka 2022/23 ambapo ni sawa na asilimia 14." Amebainisha mtaalam huyo wa Kilimo wakati akiwasilisha mada.


Katika kukabiliana na upungufu mkubwa wa mazao ya samaki Kilo ameshauri Serikali kuboresha kanuni zinazotaja nyavu zinazofaa kuvulia dagaa kwa kuweka vipimo halisi na kujenga mizani kwenye vituo vyote vya kukusanyia mazao ya uvuvi pamoja na kuwa na kanzidata ya wavuvi na kubainisha wanaojihusisha za uvuvi haramu na kuwafungia.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.