• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA MWEZI MMOJA KWA TAKUKURU KUICHUNGUZA KAMPUNI YA UJENZI MISUNGWI

Posted on: June 17th, 2025

RC MTANDA ATOA MWEZI MMOJA KWA TAKUKURU KUICHUNGUZA KAMPUNI YA UJENZI MISUNGWI


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa muda wa mwezi kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kuingia kazini kuichunguza Kampuni ya UJENZI MISUNGWI inayomilikiwa na Halmashauri kwa kushindwa kuandaa Taarifa yake hali iliyopelekea kuzalishwa kwa hoja na miradi kushindwa kutekelezwa.

Mhe. Mtanda ametoa tamko hilo mapema leo wakati akizungumza katika Baraza la Madiwani kuhusu hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi na kuwataka TAKUKURU kuharakisha uchunguzi huo ili hatua stahiki ziweze kufuatwa.

Sambamba na hilo, Mkuu wa Mkoa pia ameagiza kurudishwa kwa shilingi milioni 46 zilizotolewa kama mkopo kupitia kundi la Vijana, Aidha ametoa tahadhari kuwa wale wote waliochukua fedha hizo wazirudishe kwa wakati na hatua za kisheria zitachukuliwa kwa wale watakaoshindwa kufanya marejesho ya fedha hizo.

Kadhalika, Mkuu wa Mkoa ametoa rai kwa wawekezaji waliopatiwa viwanja na Halmashauri ambao wameshindwa kuviendeleza viwanja hivyo kuvirudisha mara moja katika umiliki wa Halmashauri ili wapewe wenye uwezo wa kuvuendeleza.

Zaidi ya hayo, Mkuu wa Mkoa ameitaka Halmashauri hiyo kufanya kazi kwa ushirikiano kati ya Wataalamu na Baraza la Madiwani ili kutokuzalisha hoja za ukaguzi.

Akiwasilisha Taarifa yake, Mwekahazina wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi CPA Andrew Ndaba amesema katika kipindi cha Mwaka wa fedha 2023/2024, Hesabu za Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi zilikaguliwa na Ofisi ya Mdhubiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, na taarifa ya ukaguzi imebainisha kuwa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi ilipata hati inayoridhisha (Unqualified Opinion).

Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ilikuwa na Jumla ya Hoja 41. Kati ya hizo hoja za miaka ya nyuma zilikuwa 14 na hoja za mwaka wa fedha 2023/2024 zilikuwa 36, zilizofungwa baada ya uhakiki ni 12 hivyo hoja zilizobaki hadi sasa ni 17. Amesema CPA Ndaba.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

    June 17, 2025
  • RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

    June 17, 2025
  • RC MTANDA ATOA MIEZI 2 KWA MANISPAA ILEMELA KUTENGENEZA MAGARI YASIYOTEMBEA

    June 17, 2025
  • RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.