• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TCRA Yaja na mfumo wa kubaini ubora wa Kampuni za Mawasiliano

Posted on: July 6th, 2019


Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) imesema imeandaa utaratibu wa kuwatuza  watoa huduma bora  za mawasiliano  nchini  lengo ikiwa  ni kuchochea ufanisi wa ubora wa huduma zinazotolewa na kampuni  za mawasiliano.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi  Mtendaji wa TCRA, Mhandisi James Kilaba wakati akizungumza na waandishi wa habari baada ya kufungwa mkutano  wa nchi   sita  za uanachama Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)  zilizokutana jijini  Mwanza kwa lengo la kujadiliana na kuweka mikakati ya pamoja juu ya gharama za kupiga simu, kuimarisha mashirika ya posta na teknolijia ya  habari na mawasiliano (TEHAMA).

Nchi hizo ni Kenya, Burundi, Rwanda, Tanzania , Uganda na Sudan Kusini ambapo watalaamu   wa TEHAMA na wajumbe wa bodi kutoka nchi hizo wamehudhuria na kuazimia mambo 11 ambayo watayatekeleza kwa mwaka mmoja na kuwasilisha utekelezaji wake mwaka 2020 watakapokutana.

Mhandisi Kilaba alisema kutokana na sekta ya mawasiliano kuwa nyenzo muhimu kwenye harakati za maendeleo itaaanza kuwatuza watoa huduma bora za mawasiliano ukiwa ni mkakati wa kuchochea ufanisi na utoaji ubora wa huduma ili kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii nchini

Alisema kutokana  na kazi kubwa  iliyofanywa na kampuni za mawasiliano  kwa kuwezesha  kuunganisha watu na kurahisisha shughuli za kijamii katika maisha ya kila siku ikiwemo biashara kupitia mfumo wa kidijitali, ni muda muafaka TCRA  kuonyesha shukrani zake.

Alisema tuzo hizo zitatolewa kwa watoa huduma kwenye sekta ya mawasiliano wa ndani ya nchi kabla ya kushirikisha nchi wanachama wa EAC.

 “Sekta ya mawasiliano nchini kupitia ubunifu wa kidijitali  umewezesha makampuni yanayoendesha biashara hiyo umeleta mapinduzi makubwa na kurahisisha maisha ya wananchi na hivyo kuchangia kukua kwa shughuli za kijamii na kiuchumi.

 “Tuzo hizo zitawafanya watoa huduma waone kufanya kazi pamoja na mamlaka , watajua mchango wao unathaminiwa, watanufaika na maboresho ikizingatiwa ushindani utakuwa endelevu,”alisema.

Awali, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Isaack Kamwelwe alifungua mkutano wa 23 wa Taasisi ya Mawasiliano ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC)  na kusema sekta ya mawasiliano  kwa muda mrefu  imekuwa ni nyenzo nzuri ya kila eneo la masilahi ya wananchi.

“Tuzo zitachochea ufanisi na kwa miaka 20 hatujafikiria kuwatuza watoa huduma wetu wa sekta ya mawasiliano, kutokana na kugusa wananchi wa maeneo mbalimbali mijini na vijijini.

“ Serikali imekubali utoaji wa tuzo hizo kwa watoa huduma na utasaidia kutoa unafuu kwa watumia huduma za mawasiliano katika dunia ya sasa ya uchumi wa kidjitali.

Aalisema mitandao ni muhimu na ndio uchumi wenyewe ikizingatiwa fedha nyingi zinatembea kwenye mifumo hiyo mbalimbali ikiwemo ndege, meli na maeneo mengine hivyo nchi haiwezi kufanikiwa kwenye uchumi wa kidijitali bila mitandao.

Mkutano huo wa 23 wa EACO uliofanyika wenye ukumbi wa Chuo cha Benki Kuu ya Tanzania (BOT),Tawi la Mwanza na kushirikisha 150 kutoka nchi sita wanachama wa EAC.






Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.