• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Uchakavu Shule kongwe Wagharimu Bilioni 19.2

Posted on: July 27th, 2019


Serikali  imesema  haitarajii kuona ndani ya miaka 10 kunatokea tena uchakavu wa rejareja wa majengo ya shule  17 kongwe nchini ambayo yamefanyiwa ukarabati mkubwa uliogharamu kiasi cha  Sh bilioni  19.2 ambazo ni kodi ya watanzania.

Hivyo imewataka wakuu wa shule, bodi na kamati za shule  kuhakikisha zinawajibika kutunza na kusimamia  rasilimali  hizo kikamilifu  na inapotokea  uharibifu wa aina yoyote ile ukiwamo kioo kunyofoka  hatua zichukuliwe haraka ili kuepuka  hasara  kubwa.

Kauli hiyo imetolewa   Mkoani Mwanza na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa  Joyce Ndalichako wakati akikiagua na kupokea majengo ya shule ya sekondari ya  Bwiru wasichana na Sengerema wavulana yaliyofanyiwa ukarabati chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).

Profesa Ndalichako alisema Serikali imetumia kiasi kikubwa kukarabati  na kujenga baadhi ya  majengo mapya katika shule kongwe 17 nchini, hivyo ni wajibu wa watumishi wa umma kuyatunza ili yaweze kutumika kuzalisha taaluma  bora kwa wanafunzi.

“Serikali iliamua kuboresha majengo ya shule kongwe hapa nchini, nakumbuka mwaka 2016 tulianza na shule 10 kwa kutumia wakandarasi lakini baadaye tulibaini  kuna gharama na kazi inachelewa kukamilika, katika awamu ya pili tuliamua kubadilisha mfumo na kuja na  ujenzi shirikishi kwa jamii ambapo tulitumia wataalamu wetu wa  vyuo vya sayansi kutushauri  na tumefanikiwa.

“Awamu hiyo ya pili tulitenga fedha  tena kwa shule saba zikiwamo ya Sengerema Wavulana na Bwiru za hapa Mwanza, hakika kazi imefanyika nzuri sana ambayo hatukututegemea kwani baadhi ya fedha zilibaki na zikatumika kujenga majengo mengine mapya, pongezi hizi ziende kwa TEA ambayo  ilipewa kazi kusimamia sughuli hii, wameonyesha uzalendo na utendaji uliotukaka.

“Rais wetu Mhe. Dkt. John Magufuli anataka kodi ya watanzania ifanye vitu vinavyoonekana kwa macho ya watu wote, ndiyo maana mnashuhuhudia miradi inaibuliwa ambayo kila mmoja anaiona na inatekelezwa kwa faida ya watu wote, wito wetu kwa wakuu wa shule na kamati na bodi zote, hatutaki kuona uchakavu wa rejareja eti kioo kimenyofoka mnakaa kimya bila hatua, hatutarajii ndani ya miaka 10 jengo limechakaa kila mmoja awajibike kuyatunza na yatumike kuinua taaluma kwa wanafunzi,”alisema.

Profesa Ndalichako alisema si kwamba shule kongwe zipo 17 nchini zilizochakaa, la hasha bali wameanza na hizo na wataendelea na zingine 82 kadri fedha zitakavyopatikana ikiwa lengo ni kutaka kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu ili watanzania wapate taaluma yenye viwango na watumishi wafanye kazi mazingira yanayovutia.

Vile Vile alisema Serikali imeanza kukarabati na kujenga majengo mapya katika vyuo vikuu vyote nchini ikiwa lengo ni lile lile  la  kuboresha miundombinu ya sekta ya elimu  ambapo aliahidi kwamba miaka miachache ijayo kilio cha nyumba za walimu kitaisha kwani wamejipanga kuondoa changamoto hiyo.

Akikabidhi majengo hayo kwa Profesa Ndalichako, Mkurugenzi Mtendaji wa TEA, Bahati Geuze, aliishukuru Serikali kwa kuwaamini kusimamia ukarabati wa shule kongwe nchini na shughuli hiyo wameifanya kwa uadilifu mkubwa sana.

Alisema gharama zilizotumika kukarabati na kujenga baadhi ya majengo mapya katika shule kongwe 17  chini ni Sh bilioni 19.28 ambapo kwa  upande wa sekondari ya wasichana zilitumika Sh. milioni 974 huku Sengerena wavulana zilitumika Sh bilioni 1.2.

“TEA inaahidi kuendelea kukarabati shule zilizochakaa na  kufuatilia kwa ukaribu  miradi ya shule, moja ya changamoto iliyokuwa ikitukabili wakati wa utekelezaji ni baadhi ya shule gharama kuongezeka kwani unaponza kuboresha eneo moja, tatizo linguine linajitokeza tena hivyo lazima litatutuliwe ili ujenzi uendelee,”alisema.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.