• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

DKT. NCHEMBA ATOA POLE KWA WANANCHI WALIOHARIBIWA MALI KUTOKANA NA VURUGU MKOANI MWANZA

Posted on: December 5th, 2025

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (MB) ametoa pole kwa wananchi wa Mkoa wa Mwanza kwa kuharibiwa mali zao, kusababishiwa hasara na kukosa huduma muhimu za kijamii.

Dkt. Nchemba ametoa pole hiyo wakati akikagua Kiwanda cha magodoro cha Banco pamoja na Ofisi ya Maboto microfinance katika Wilaya za Nyamagana na Ilemela ikiwa ni miongoni mwa mali za wananchi zilizoharibiwa katika vurugu zilizojitokeza Octoba, 29, 2025.

Dkt. Nchemba amesema kuwa analaani vitendo vya uvunjifu wa amani na vurugu zinazorudisha nyuma amani kwani kwa kipindi kirefu Tanzania imekua ikifahamika kama kisiwa cha utulivu.

Aidha amewataka wananchi kujutia matendo waliyoyafanya na ametoa wito kwa kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzie na kuhakikisha vijana wanakemewa kwa matendo hayo kwani yana madhara makubwa kwa taifa.

Sambamba na hayo Dkt. Nchemba amesema baada ya kufanyika tathmini ya kina juu ya uharibifu uliofanyika, serikali itatoa tamko rasmi kuhusu hatua zipi zitachukuliwa pia ameahidi kuwa, watahakikisha wanaimarisha maswala ya kiusalama katika nchi ili kuhakikisha uharibifu wa namna hio haujitokezi tena.

Akikagua uharibifu uliofanywa kwenye ofisi ya mtendaji wa kata ya Nyasaka wilayani Ilemela Dkt. Nchemba amewataka wananchi kutokubali kurubuniwa na watu wasioitakia mema nchi.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema uharibifu wa ofisi ya mtendaji wa kata hio ya Nyasaka umepelekea wananchi zaidi ya elfu 41 kukosa huduma huku uongozi wa kata ukipata hasara ya Shilingi milioni 35.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA AMEWATAKA WAHITIMU IFM KUWA MABALOZI WAZURI WA CHUO CHAO

    December 06, 2025
  • RC MTANDA AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZINAZOPATIKANA

    December 06, 2025
  • SERIKALI YATENGA FEDHA KUKAMILISHA MIRADI YA MAENDELEO MWANZA - DKT. NCHEMBA

    December 05, 2025
  • DKT. NCHEMBA ATOA POLE KWA WANANCHI WALIOHARIBIWA MALI KUTOKANA NA VURUGU MKOANI MWANZA

    December 05, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.